WATAHINIWA 67 WA KIDATO CHA NNE 2024,WAFUTIWA MATOKEO | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

WATAHINIWA 67 WA KIDATO CHA NNE 2024,WAFUTIWA MATOKEO

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limewafutia matokeo watahiniwa 67 waliofanya udanganyifu wakati wa mtihani wa Taifa wa kidato cha nne uliofanyika Novemba mwaka 2024 huku ikikifungia kituo cha mtihani chenye namba za usajili p6384 BSL Open School kilichopo mkoa wa Shinyanga kuwa kituo cha mitihani ya Taifa kutokana mipango ya udanganyifu.

Sophia Kingimali.
By Sophia Kingimali.
23 Jan 2025
WATAHINIWA 67 WA KIDATO CHA NNE 2024,WAFUTIWA MATOKEO

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limewafutia matokeo  watahiniwa 67 waliofanya udanganyifu  wakati wa  mtihani wa Taifa wa kidato cha nne uliofanyika Novemba mwaka 2024 huku ikikifungia kituo cha mtihani chenye namba za usajili p6384 BSL Open School  kilichopo mkoa wa Shinyanga  kuwa  kituo cha mitihani ya Taifa  kutokana  mipango  ya udanganyifu.

Akitangaza matokeo hayo leo, Januari, 25  2025 jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa NECTA,Dk. Said Mohamed  amesema  katika idadi hiyo  wapo wanafunzi walioandika lugha ya matusi katika karatasi  zao za mtihani wa kidato cha nne.

"Matokeo  haya yamefutwa kwa mujibu  wa kifungu cha 5 (2) (j) cha Sheria ya Baraza la Mitihani  sura ya 107 kikisomwa pamoja  na kifungu  cha 30(2) (b) cha Kanuni za Mitihani  mwaka 2016," amesema Dk. Mohamed.

Aidha ameongeza kuwa  NECTA imezuia kutoa  matokeo ya watahiniwa  459 ambao walipata matatizo  ya kiafya  na kushindwa kufanya mtihani  wa kidato  cha nne 2024 kwa masomo yote au idadi  kubwa ya masomo.

Amesema watahiniwa  husika  wamepewa fursa  ya kufanya  mtihani  kwa masomo ambayo  hawakufanya kwa sababu ya ugonjwa mwaka 2025 kwa mujibu wa  kifungu cha 32 (1) cha Kanuni za mtihani.

" kituo hiki kimefungwa kwa mujibu  wa kifungu 4 (8) cha kanuni  za mtihani mwaka 2016 hadi hapo Baraza  litakapojiridhisha kuwa ni salama kwa uendeshaji wa Mitihani  ya Taifa, " amesema

GHARAMA YA KUPANDIKIZA MIMBA NI MILIONI 14 MUHIMBILI.

GHARAMA YA KUPANDIKIZA MIMBA NI MILIONI 14 MUHIMBILI.

MOI Imefanikiwa Kuanzisha Huduma Zaidi ya 10 lkiwemo Upasuaji wa Ubongo Bila Kufungua Fuvu.

MOI Imefanikiwa Kuanzisha Huduma Zaidi ya 10 lkiwemo Upasuaji wa Ubongo Bila Kufungua Fuvu.

WANANCHI WAILILIA SERIKALI,WAFUKUZWA KWENYE MAENEO YAO.

WANANCHI WAILILIA SERIKALI,WAFUKUZWA KWENYE MAENEO YAO.

RIKA LINALOTAKA KUPANDIKIZWA MIMBA NI KUANZIA MIAKA 35 HADI 50.

RIKA LINALOTAKA KUPANDIKIZWA MIMBA NI KUANZIA MIAKA 35 HADI 50.

Vikundi 21 kunufaika na Mradi wa Tuinuke Pamoja Kukuza Usawa wa Kijinsia Kondoa, Chemba

Vikundi 21 kunufaika na Mradi wa Tuinuke Pamoja Kukuza Usawa wa Kijinsia Kondoa, Chemba