

Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), imeendelea kuwahamasisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika maeneo maalum ya kiuchumi yaliyotengwa na Serikali ambapo katika eneo la Nala, jumla ya wawekezaji wazawa wanne wameonesha utayari wa kuwekeza
Hayo yameelezwa leo Septemba 23, 2025 na Meneja wa Kanda ya Kati wa Mamlaka hiyo, Venance Mashiba mbele ya Wandishi wa Habari waliotembelea eneo la uwekezaji la Nala lililopo jijini Dodoma ikiwa ni programu iliyoandaliwa na TISEZA kwa ajili ya kutoa elimu kwa Waandishi hao ili wapate uelewa wa maeneo hayo na kuendelea kuhamasisha uwekezaji kupitia vyombo vya habari.
Meneja Mashiba amesema kuwa, wamewapeleka Waandishi wa Habari katika eneo hilo ili wajionee eneo lilivyo na mazingira yaliyowekwa na serikali kwa ajili ya kuvutia uwekezaji.
"Tunaendelea kuhamasisha wawekezaji wengi kuwekeza hapa Nala kwani maeneo haya yana huduma zote muhimu, mpaka sasa tuna kiwanda kimoja ambacho ujenzi wake unakaribia kukamilika na wawekezaji wanne wazawa wameleta maombi ya kupatiwa maeneo. Pia, tunaendelea na mazungumzo na wawekezaji wa nje. Tunatoa rai kwenu Waandishi wa Habari kutusaidia kuhamasisha kupitia vyombo vya habari ", amesema Meneja Mashiba.
Amewaeleza Waandishi hao sifa ambazo zimetolewa na Mamlaka hiyo kwa wawekezaji wanaohitaji nafasi hiyo kuwa ni uwekezaji uwe na thamani isiyopungua Dola za Marekani milioni 5 kwa muwekezaji wa ndani na uwekezaji usiopungua thamani ya Dola za Marekani milioni 10 kwa muwekezaji kutoka nje, uwekezaji kuweza kutoa ajira za moja kwa moja zaidi ya 100 pamoja na kuwa na teknolojia za kisasa.
Kwa upande wake, Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Mamlaka hiyo, Pendo Gondwe amesema kuwa eneo hilo lina jumla ya hekta 607 ambalo litakuwa na viwanda mbalimbali vikiwemo vya dawa, usindikaji wa mazao, utengenezaji wa magari na miradi ya teknolojia na viwanda vingine ambapo matarajio ya serikali ni kulifanya eneo hilo kuwa na viwanda vingi ifikapo mwaka 2030.
"Tunahakikisha tunatangaza fursa kwa Watanzania watakaohitaji kuwekeza, tunatarajia itakapofika Disemba angalau viwanda 100 viwepo kwenye maeneo maalum ya kiuchumi ikiwemo Nala", amesema Pendo.
Amesisitiza kuwa, Serikali imetoa ardhi bure ili kuhamasisha uwekezaji wa haraka ambapo muwekezaji atatakiwa kujenga kiwanda ndani ya mwaka mmoja. Ametaja vivutio vingine vya uwekezaji katika maeneo maalum kuwa ni pamoja na kuondolewa kodi kwenye baadhi ya maeneo na kupunguziwa kodi kwenye uingizaji wa mitambo na malighafi.
Mfalme wa Mashairi Awasha Moto wa Uzalendo: “Kura Yako Ni Silaha”
MUFTI ATAKA WAISLAMU KUZINGATIA MAFUNDISHO YA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29.
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA KUWAKATAA WASIOHESHIMU MISINGI NA TUNU ZA NCHI
Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha
BADO TUNAMUHITAJI POLEPOLE KWA MKURUGENZI WA UPELELEZI- POLISI
BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA
Mkomi Awasisitiza Wakuu wa Taasisi Kusimamia Mifumo ya Kielektroniki Serikalini.
WAZEE WAASWA KUHAMASISHA JAMII KUJITOKEZA KUPIGA KURA.
JAMII YAHIMIZWA KUWAKATAA WANAOTAFUTA HAKI KWA KUVUNJA SHERIA