

WATANZANIA wametakiwa kushiriki katika shindano la kidigital la huduma za kifedha ili kuweza kuibuka washindi na kubadilisha historia za maisha yao lakini pia kukuza matumizi fedha kidigital.
WATANZANIA wametakiwa kushiriki katika shindano la kidigital la huduma za kifedha ili kuweza kuibuka washindi na kubadilisha historia za maisha yao lakini pia kukuza matumizi fedha kidigital.
Pia,wanafunzi wa vyuo wametakiwa kutumia huduma za simbanking ili kuweza kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo ufadhili wa masomo na fedha taslimu.
Fahad Soud, MKAZI wa Jiji la Tanga,ameibuka mshindi wa pili wa gari jipya aina ya IST kupitia kampeni ya Benki ya CRDB inayolenga kuhamasisha matumizi ya huduma za kidijitali, hususan SimBanking.
Akizungumza katika Hafla ya makabidhiano ya zawadi hiyo ilifanyika katika Viwanja vya Dar Village, Mikocheni jijini Dar es Salaam ambapo ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa benki hiyo na wadau mbalimbali,Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa CRDB, Stephen Adili, amesema kampeni hiyo ni sehemu ya kurudisha fadhila kwa wateja wanaotumia huduma za kidijitali za benki hiyo.
“Mbali na magari aina ya IST yanayotolewa kila mwezi, zawadi nyingine mbalimbali kama fedha taslimu pia zinapatikana. Ili kushiriki, mteja anatakiwa kuwa na akaunti ya CRDB na amejiunga na SimBanking. Kila muamala unakupa nafasi ya kushinda, iwe ni kununua umeme, kulipia bili au kukata tiketi za SGR,” amesema Adili.
Adili amesisitiza kuwa huduma ya SimBanking ni jumuishi na haina mipaka kwa kundi maalumu la wateja, kwani inawahusu makundi yote wakimo wanafunzi, wafanyabiashara, watumishi wa umma na hata wafanyakazi binafsi.
Kwa upande wake, mshindi wa zawadi hiyo, Fahad Soud, aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuendesha kampeni hiyo na kuwataka wateja wengine kujitokeza kwa wingi kutumia SimBanking.
“Nimefurahi sana kushinda gari kupitia huduma hii. Naomba Watanzania waamini kwamba kampeni hii ni ya kweli na washiriki kwa kufanya miamala kupitia SimBanking ili nao waweze kushinda kama mimi,” alisema Fahad.
Kwa mujibu wa CRDB, droo hiyo itaendelea hadi mwezi Disemba ambapo mshindi wa mwisho atajinyakulia gari aina ya Harrier Anaconda, huku wateja wengine wakiendelea kujipatia zawadi mbalimbali kila mwezi.
Mfalme wa Mashairi Awasha Moto wa Uzalendo: “Kura Yako Ni Silaha”
MUFTI ATAKA WAISLAMU KUZINGATIA MAFUNDISHO YA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29.
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA KUWAKATAA WASIOHESHIMU MISINGI NA TUNU ZA NCHI
Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha
BADO TUNAMUHITAJI POLEPOLE KWA MKURUGENZI WA UPELELEZI- POLISI
BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA
Mkomi Awasisitiza Wakuu wa Taasisi Kusimamia Mifumo ya Kielektroniki Serikalini.
WAZEE WAASWA KUHAMASISHA JAMII KUJITOKEZA KUPIGA KURA.
JAMII YAHIMIZWA KUWAKATAA WANAOTAFUTA HAKI KWA KUVUNJA SHERIA