CRDB WATOA GARI LA PILI KWA MSHINDI,WATANZANIA WAHAMASISHWA KUCHANGAMKIA FURSA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Biashara

CRDB WATOA GARI LA PILI KWA MSHINDI,WATANZANIA WAHAMASISHWA KUCHANGAMKIA FURSA.

WATANZANIA wametakiwa kushiriki katika shindano la kidigital la huduma za kifedha ili kuweza kuibuka washindi na kubadilisha historia za maisha yao lakini pia kukuza matumizi fedha kidigital.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
19 Sep 2025
CRDB WATOA GARI LA PILI KWA MSHINDI,WATANZANIA WAHAMASISHWA KUCHANGAMKIA FURSA.

WATANZANIA wametakiwa kushiriki katika shindano la kidigital la huduma za kifedha ili kuweza kuibuka washindi na kubadilisha historia za maisha yao lakini pia kukuza matumizi fedha kidigital.

Pia,wanafunzi wa vyuo wametakiwa kutumia huduma za simbanking ili kuweza kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo ufadhili wa masomo na fedha taslimu.

Fahad Soud, MKAZI wa Jiji la Tanga,ameibuka mshindi wa pili wa gari jipya aina ya IST kupitia kampeni ya Benki ya CRDB inayolenga kuhamasisha matumizi ya huduma za kidijitali, hususan SimBanking.

Akizungumza katika Hafla ya makabidhiano ya zawadi hiyo ilifanyika katika Viwanja vya Dar Village, Mikocheni jijini Dar es Salaam ambapo ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa benki hiyo na wadau mbalimbali,Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa CRDB, Stephen Adili, amesema kampeni hiyo ni sehemu ya kurudisha fadhila kwa wateja wanaotumia huduma za kidijitali za benki hiyo.

“Mbali na magari aina ya IST yanayotolewa kila mwezi, zawadi nyingine mbalimbali kama fedha taslimu pia zinapatikana. Ili kushiriki, mteja anatakiwa kuwa na akaunti ya CRDB na amejiunga na SimBanking. Kila muamala unakupa nafasi ya kushinda, iwe ni kununua umeme, kulipia bili au kukata tiketi za SGR,” amesema Adili.

Adili amesisitiza kuwa huduma ya SimBanking ni jumuishi na haina mipaka kwa kundi maalumu la wateja, kwani inawahusu makundi yote wakimo wanafunzi, wafanyabiashara, watumishi wa umma na hata wafanyakazi binafsi.

Kwa upande wake, mshindi wa zawadi hiyo, Fahad Soud, aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuendesha kampeni hiyo na kuwataka wateja wengine kujitokeza kwa wingi kutumia SimBanking.

“Nimefurahi sana kushinda gari kupitia huduma hii. Naomba Watanzania waamini kwamba kampeni hii ni ya kweli na washiriki kwa kufanya miamala kupitia SimBanking ili nao waweze kushinda kama mimi,” alisema Fahad.

Kwa mujibu wa CRDB, droo hiyo itaendelea hadi mwezi Disemba ambapo mshindi wa mwisho atajinyakulia gari aina ya Harrier Anaconda, huku wateja wengine wakiendelea kujipatia zawadi mbalimbali kila mwezi.


 


 


 


 


 


 

FCC  YAIMARISHA USHIRIKIANO NA TUME YA USHINDANI YA AFRIKA KUSINI

FCC YAIMARISHA USHIRIKIANO NA TUME YA USHINDANI YA AFRIKA KUSINI

DC Nyamwese aanika fursa za uwekezaji Handeni

DC Nyamwese aanika fursa za uwekezaji Handeni

Nala Dodoma Kuwa Kitovu cha Viwanda, Wawekezaji Wajitokeza

Nala Dodoma Kuwa Kitovu cha Viwanda, Wawekezaji Wajitokeza

Kodi Sasa Si Kikwazo: Wafanyabiashara Wazidi Kuunga Mkono Serikali.

Kodi Sasa Si Kikwazo: Wafanyabiashara Wazidi Kuunga Mkono Serikali.

BRELA YAFANYA KAZI NZURI YA URASIMISHAJI BIASHARA MWANZA

BRELA YAFANYA KAZI NZURI YA URASIMISHAJI BIASHARA MWANZA