JAMII YAHIMIZWA KUWAKATAA WANAOTAFUTA HAKI KWA KUVUNJA SHERIA | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

JAMII YAHIMIZWA KUWAKATAA WANAOTAFUTA HAKI KWA KUVUNJA SHERIA

Jamii imesisitizwa kujitokeza kwa Wingi Oktoba 29, 2025 na kupiga kura kuwachagua Viongozi wanaofaa na wanaoweza kuwaletea maendeleo ya kweli kama sehemu ya kutimiza Haki ya kila Mwananchi Kikatiba lakini pia katika kuamua hatma ya maisha ya Kila mmoja katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
06 Oct 2025
JAMII YAHIMIZWA KUWAKATAA WANAOTAFUTA HAKI KWA KUVUNJA SHERIA

Jamii imesisitizwa kujitokeza kwa Wingi Oktoba 29, 2025 na kupiga kura kuwachagua Viongozi wanaofaa na wanaoweza kuwaletea maendeleo ya kweli kama sehemu ya kutimiza Haki ya kila Mwananchi Kikatiba lakini pia katika kuamua hatma ya maisha ya Kila mmoja katika kipindi cha miaka mitano ijayo.

Wito huo umetolewa na Wananchi wa Tabata Jijini Dar Es Salaam leo Jumatatu Oktoba 06, 2025 wakati wakizungumza na Mwandishi wetu wa habari, wakisisitiza pia kila mmoja kufanya tafakuri na kutokubali kurubuniwa na kujiingiza kwenye maandamano yanayoratibiwa na kuhamasishwa na watu wasiokuwa nchini na wasioitakia mema Tanzania.

Ally Kazimoto ni mmoja wa waliozungumza nasi ambapo ametanabainisha kujiandaa vyema kushiriki katika uchaguzi Mkuu ujao na kuhamasisha Vijana wenzake kutorubuniwa kuandamana, akisema ni muhimu kabla ya kuandamana kujiuliza athari za maandamano hayo,akisisitiza kuwa haki haidaiwi kwa kuvunja sheria na miongozo iliyopo nchini.

Kwa upande wake Raskazia Mwita na Hamis Maneno, wamewasihi Vijana na Wanawake kutafakati hatma ya Watoto na familia zao kabla ya kuandamana hiyo Oktoba 29, wakieleza kuwa ni ubinafsi kuandamana bila kujali haki na usalama wa wengine kwani maandamano ya Oktoba ni batili na hayakubaliki kutokana na Serikali kuitenga siku hiyo kuwa maalumu kwaajili ya uchaguzi mkuu peke yake.

DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”

DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”

VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA KUWAKATAA WASIOHESHIMU MISINGI NA TUNU ZA NCHI

VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA KUWAKATAA WASIOHESHIMU MISINGI NA TUNU ZA NCHI

VIJANA WATAKIWA KUCHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTIMIZA MATARAJIO YAO

VIJANA WATAKIWA KUCHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTIMIZA MATARAJIO YAO

MKURANGA WAPO TAYARI KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU KWA AMANI

MKURANGA WAPO TAYARI KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU KWA AMANI

BAKWATA MWANZA YAWAHIMIZA WAUMINI WAKE KUANZA MFUNGO KUOMBEA AMANI YA TANZANIA

BAKWATA MWANZA YAWAHIMIZA WAUMINI WAKE KUANZA MFUNGO KUOMBEA AMANI YA TANZANIA