

Jamii imesisitizwa kujitokeza kwa Wingi Oktoba 29, 2025 na kupiga kura kuwachagua Viongozi wanaofaa na wanaoweza kuwaletea maendeleo ya kweli kama sehemu ya kutimiza Haki ya kila Mwananchi Kikatiba lakini pia katika kuamua hatma ya maisha ya Kila mmoja katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Jamii imesisitizwa kujitokeza kwa Wingi Oktoba 29, 2025 na kupiga kura kuwachagua Viongozi wanaofaa na wanaoweza kuwaletea maendeleo ya kweli kama sehemu ya kutimiza Haki ya kila Mwananchi Kikatiba lakini pia katika kuamua hatma ya maisha ya Kila mmoja katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Wito huo umetolewa na Wananchi wa Tabata Jijini Dar Es Salaam leo Jumatatu Oktoba 06, 2025 wakati wakizungumza na Mwandishi wetu wa habari, wakisisitiza pia kila mmoja kufanya tafakuri na kutokubali kurubuniwa na kujiingiza kwenye maandamano yanayoratibiwa na kuhamasishwa na watu wasiokuwa nchini na wasioitakia mema Tanzania.
Ally Kazimoto ni mmoja wa waliozungumza nasi ambapo ametanabainisha kujiandaa vyema kushiriki katika uchaguzi Mkuu ujao na kuhamasisha Vijana wenzake kutorubuniwa kuandamana, akisema ni muhimu kabla ya kuandamana kujiuliza athari za maandamano hayo,akisisitiza kuwa haki haidaiwi kwa kuvunja sheria na miongozo iliyopo nchini.
Kwa upande wake Raskazia Mwita na Hamis Maneno, wamewasihi Vijana na Wanawake kutafakati hatma ya Watoto na familia zao kabla ya kuandamana hiyo Oktoba 29, wakieleza kuwa ni ubinafsi kuandamana bila kujali haki na usalama wa wengine kwani maandamano ya Oktoba ni batili na hayakubaliki kutokana na Serikali kuitenga siku hiyo kuwa maalumu kwaajili ya uchaguzi mkuu peke yake.
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA KUWAKATAA WASIOHESHIMU MISINGI NA TUNU ZA NCHI
Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha
HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA
TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO
BADO TUNAMUHITAJI POLEPOLE KWA MKURUGENZI WA UPELELEZI- POLISI
BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA
Mkomi Awasisitiza Wakuu wa Taasisi Kusimamia Mifumo ya Kielektroniki Serikalini.
WAZEE WAASWA KUHAMASISHA JAMII KUJITOKEZA KUPIGA KURA.
CRDB YAZINDUA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA HUKU WAKIJIVUNIA MAFANIKIO MAKUBWA KWA MIAKA 30