HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA

Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania Bw. Gerson Msigwa amewahakikishia Watanzania wote wenye sifa na waliojiandikisha kwenye daftari na mpiga kura kuwa serikali ya awamu ya sita inatambua kikamilifu wajibu wake wa kulinda haki ya kila Mtanzania ikiwemo haki ya Kikatiba ya Kuchagua na kuchaguliwa, akiwahimiza kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo Oktoba 29, 2025.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
13 Oct 2025
HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA

Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania Bw. Gerson Msigwa amewahakikishia Watanzania wote wenye sifa na waliojiandikisha kwenye daftari na mpiga kura kuwa serikali ya awamu ya sita inatambua kikamilifu wajibu wake wa kulinda haki ya kila Mtanzania ikiwemo haki ya Kikatiba ya Kuchagua na kuchaguliwa, akiwahimiza kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo Oktoba 29, 2025.

Msemaji huyo wa serikali amewatoa hofu pia Watanzania dhidi ya yale yanayosemwa mtandaoni kuelekea siku ya uchaguzi Mkuu wa Tanzania, akisema serikali na Vyombo vya Dola vimejipanga na kujiandaa kikamilifu kuhakikisha kuwa uchaguzi unafanyika kwa amani na katika mazingira tulivu na salama ili kutoa fursa ya kila mmoja kuitumia haki yake ya Kikatiba.

"Naomba niwahakikishie Watanzania wote kuwa amani ipo tena ya kutosha kwahiyo msiwe na wasiwasi wowote serikali hii ni makini, Vyombo vyetu vyote vya Dola vimejiandaa kikamilifu kuhakikisha utulivu na amani ya kutosha. Nenda kachague Kiongozi unayemtaka na hakuna mtu yoyote atakayefanya chochote. Achaneni na maneno yanayotengenezwa mtandaoni kuwatishia watu na kuwaaminisha vitu ambavyo havitatokea." Amesema Msigwa.

Aidha Msigwa pia amehimiza watanzania kuendelea kujiandaa na upigaji huo wa kura kwa kusikiliza mikutano ya Kampeni ya Wagombea Udiwani, Ubunge na Urais wa Tanzania ili kuwa na maamuzi sahihi ya kuchagua Kiongozi anayefaa badala ya kusubiri kuchaguliwa Kiongozi wa eneo lako na watu wengine.

Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha

Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO

Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya  VSOMO ya VETA

Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya VSOMO ya VETA

WENYE ULEMAVU WAHAMASISHA KUJITOKEZA KUWACHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTETEA MASLAHI YAO

WENYE ULEMAVU WAHAMASISHA KUJITOKEZA KUWACHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTETEA MASLAHI YAO

BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA

BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA