Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ametoa wiki moja kwa uongozi wa TANESCO kufanya maboresho ya Kituo cha huduma kwa wateja na matokeo yake yawe wazi kwa Wananchi lakini pia ameagiza kufumuliwa kwa Kituo hicho kufuatia kituo kushindwa kuwahudumia Wananchi kwa viwango vinavyotarajiwa.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko ametoa wiki moja kwa uongozi wa TANESCO kufanya maboresho ya Kituo cha huduma kwa wateja na matokeo yake yawe wazi kwa Wananchi lakini pia ameagiza kufumuliwa kwa Kituo hicho kufuatia kituo kushindwa kuwahudumia Wananchi kwa viwango vinavyotarajiwa.
Maagizo hayo ameyatoa leo Januari 9,2025 jijini Dar es Salaam baada ya kutembelea kituo hicho pamoja na mambo mengine lakini pia kufuatilia utekelezaji wa maelekezo yake aliyoyatoa mwezi Aprili, 2024.
Dkt. Biteko ameshangazwa na hatua ya TANESCO kuweka kando maelekezo yake ya mwezi Aprili 2024 yaliyolitaka Shirika hilo kuondokana na matumizi ya namba za kulipia kwenye utoaji wa huduma na kuomba namba ya bure ya huduma (free toll number) kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ili kuwapa unafuu wananchi wanaohitaji huduma za TANESCO.
" Wewe ulishapiga simu, pesa yako ikakatwa na huduma usiipate? Wananchi wanaumia sana!" naagiza kuundwa upya kituo ili kuongeza ufanisi na tija kwa Wananchi, "kituo hiki kinategemewa na Watanzania wengi na huduma inayotolewa hapa hairidhishi kabisa," amesema Dkt. Biteko.
Ameongeza kuwa, Serikali ya Rais Samia imetoa fedha nyingi kuhudumia kituo hicho lakini utendaji wake ni mbovu kuliko huduma ya kituo.
TANESCO ilielekezwa kuachana na matumizi ya namba za kulipia Kwenye utoaji wa huduma na kuomba namba ya bure ya huduma (toll number) kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania-TCRA ili kuwapa unafuu wa Wananchi wanapopiga kuhitaji huduma za TANESCO.
Akizungumzia utendaji wa Kituo hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mha. Abubakar Issa amesema kulikuwa na changamoto za kibajeti. Hivyo ameahidi kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA watakaa haraka na kuanza matumizi ya namba bila malipo ili kutoa unafuu kwa wananchi na kuleta tija kwa watumiaji.
WAGOMBEA NAFASI YA NGAZI YA URAIS CCM KUTAMBULISHWA KWENYE MIAKA 48 YA CHAMA HICHO.
SERIKALI KUFANYA SENSA YA UZALISHAJI VIWANDA KWA MWAKA WA REJEA 2023.
AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MABADILIKO YA SERA YA ELIMU KUAKISI MABADILIKO YA KITAIFA NA KIMATAIFA.
RASMI UZINDUZI WA SERA YA ELIMU KUFANYIKA TAREHE 1 FEBRUARI 2025.
WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.