WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema Chama na serikali yake haitakubaliana na azimio lolote litakalotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) baada ya kukutana kwa faragha kama walivyotangaza viongozi wa chama hicho, juzi.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
30 Jan 2025
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.

Amesema amesikia chama hicho kikitangaza kwamba kinakwenda kujifungia kisha kije na jambo ambalo halijapata kushuhudiwa nchini, hivyo ametoa angalizo jambo hilo ni lazima lifuate sharia za nchi.

Wasira amesema hayo leo alipohutubia wananchi katika mkutano uliotumika kuzindua sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya kuzaliwa kwa Chama kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Stendi ya Zamani mjini Bunda.

“Wamesema wanajifungia halafu waje wafanye jambo ambalo halijapata kuonekana, nikasema ni jambo gani, mimi nikaona huko kujifungia ile ni honeymoon maana honeymoon simnaijua, watu wakishaoana wanajifungia mahali…ile ni honemoon.

“Tunawaambia tunawatakia heri kwenye honeymoon lakini tunawaambia lolote watakalotoka nalo kwenye honeymoon lazima lifuate sheria, waklija na honeymoon inavunja amani hatuwezi kuwaunga mkono.

DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDS

DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDS

KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani

KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani

Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.

Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.

RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya  Migogoro ya Ardhi Nchini.

RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya Migogoro ya Ardhi Nchini.

DAWASA Imeendelea na Utekelezaji wa Miradi Zaidi ya 25 Yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 987.6.

DAWASA Imeendelea na Utekelezaji wa Miradi Zaidi ya 25 Yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 987.6.