Waziri wa Elimu sayansi na Teknolojia Mhe.Prof Adolf Mkenda ametoa taarifa kwa umma juu ya kusogezwa mbele kwa tukio la uzinduzi wa Sera ya elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la mwaka 2023 na mitaala iliyoboreshwa kuwa rasmi tukio hilo litafanyika mapema Februari mosi mwaka huu.
Ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari tarehe 30 januari 2025,kwenye ofisi za Wizara ya elimu zilizopo jijini Dodoma.
Aidha amesema kuwa anawasihi wageni ambao tayari wamekwisha anza safari waje dodoma na watapata siku Moja ya kulijua vizuri Jiji la Dodoma huku wakisubiri tukio hilo na Kwa wale ambao bado hawajaanza basi waangalie namna ya kuendana na mabadiliko.
"Tuna jua wapo walioanza safari za kuja tunaomba watuvumilie na wabaki Dodoma na ambao bado hawajaanza waweke vizuri ratiba zao ili kuenda sawa na tarehe hiyo"
Aidha tukio hilo linalosubiriwa kwa hamu lilipagwa kufanyika tarehe 31,januari mwaka huu na sasa limepelekwa mbele kwa sababu zisizozuilika amabapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan.
Mkutano huo utahusisha wadau wa elimu mbalimbali kutoka Tanzania bara na Visiwani kwani ni jambo ambalo lilikuwa likisubiriwa Kwa hamu na wadau wa Sekta ya elimu ili kujipambanua Kitaifa na kimataifa.
WAGOMBEA NAFASI YA NGAZI YA URAIS CCM KUTAMBULISHWA KWENYE MIAKA 48 YA CHAMA HICHO.
SERIKALI KUFANYA SENSA YA UZALISHAJI VIWANDA KWA MWAKA WA REJEA 2023.
AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MABADILIKO YA SERA YA ELIMU KUAKISI MABADILIKO YA KITAIFA NA KIMATAIFA.
WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.
WAGOMBEA NAFASI YA NGAZI YA URAIS CCM KUTAMBULISHWA KWENYE MIAKA 48 YA CHAMA HICHO.