RASMI UZINDUZI WA SERA YA ELIMU KUFANYIKA TAREHE 1 FEBRUARI 2025. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

RASMI UZINDUZI WA SERA YA ELIMU KUFANYIKA TAREHE 1 FEBRUARI 2025.

Waziri wa Elimu sayansi na Teknolojia Mhe.Prof Adolf Mkenda ametoa taarifa kwa umma juu ya kusogezwa mbele kwa tukio la uzinduzi wa Sera ya elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 toleo la mwaka 2023 na mitaala iliyoboreshwa kuwa rasmi tukio hilo litafanyika mapema Februari mosi mwaka huu.

Moreen Rojas, Dodoma.
By Moreen Rojas, Dodoma.
30 Jan 2025
RASMI UZINDUZI WA SERA YA ELIMU KUFANYIKA TAREHE 1 FEBRUARI 2025.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari tarehe 30 januari 2025,kwenye ofisi za Wizara ya elimu zilizopo jijini Dodoma.

Aidha amesema kuwa anawasihi wageni ambao tayari wamekwisha anza safari waje dodoma na watapata siku Moja ya kulijua vizuri Jiji la Dodoma huku wakisubiri tukio hilo na Kwa wale ambao bado hawajaanza basi waangalie namna ya kuendana na mabadiliko.

"Tuna jua wapo walioanza safari za kuja tunaomba watuvumilie na wabaki Dodoma na ambao bado hawajaanza waweke vizuri ratiba zao ili kuenda sawa na tarehe hiyo"

Aidha tukio hilo linalosubiriwa kwa hamu lilipagwa kufanyika tarehe 31,januari mwaka huu na sasa limepelekwa mbele kwa sababu zisizozuilika amabapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa ni Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan.

Mkutano huo utahusisha wadau wa elimu mbalimbali kutoka Tanzania bara na Visiwani kwani ni jambo ambalo lilikuwa likisubiriwa Kwa hamu na wadau wa Sekta ya elimu ili kujipambanua Kitaifa na kimataifa.

DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDS

DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDS

KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani

KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani

Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.

Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.

RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya  Migogoro ya Ardhi Nchini.

RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya Migogoro ya Ardhi Nchini.

DAWASA Imeendelea na Utekelezaji wa Miradi Zaidi ya 25 Yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 987.6.

DAWASA Imeendelea na Utekelezaji wa Miradi Zaidi ya 25 Yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 987.6.