Mwaimu Akutana na Kuzungumza na Ujumbe wa Balozi wa USA Nchini | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kimataifa

Mwaimu Akutana na Kuzungumza na Ujumbe wa Balozi wa USA Nchini

Septemba 7, 2023 Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mathew Mwaimu (Jaji Mstaafu) amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Balozi wa Marekani nchini Tanzania, ulipotembelea Makao Makuu ya Ofisi za Tume zilizopo mtaa wa Kilimani jijini Dodoma.

Winner Marawiti
By Winner Marawiti
08 Sep 2023
Mwaimu Akutana na Kuzungumza na Ujumbe wa Balozi wa USA Nchini

Ujumbe huo wa watu watatu uliongozwa na Mshauri wa masuala ya Siasa na Uchumi katika Ubalozi huo, Bwana Jonathan Howard aliyeambatana na Bwana Andy Allen  na Bi. Beatrice.

Katika mazungumzo yao Ujumbe huo ulipata fursa ya kuifahamu zaidi Tume na majukumu yake na   Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu.

Pia, katika mazungumzo yao viongozi hao walijadili maeneo mbalimbali ya mashirikiano kwa lengo la kukuza na kulinda haki za binadamu nchini.

Mkurugenzi wa  Malalamiko na Uchunguzi, Bi. Suzana  Pascal aliambatana na Mwenyekiti wa Tume katika mazungumzo hayo.

Profesa Malebo:Tanzania  inatoa uhuru wa kujieleza na hakuna vitisho wala unyanyasaji wa wananchi

Profesa Malebo:Tanzania inatoa uhuru wa kujieleza na hakuna vitisho wala unyanyasaji wa wananchi

MPANGO afungua mkutano wa kumi wa wakaguzi wa ndani Afrika

MPANGO afungua mkutano wa kumi wa wakaguzi wa ndani Afrika

RAIS DKT.SAMIA AANDALIWA DHIFA YA KITAIFA NORWAY

RAIS DKT.SAMIA AANDALIWA DHIFA YA KITAIFA NORWAY

Ni Aibu Afrika Kulia Ukosefu wa Chakula-Rais Dkt. Samia

Ni Aibu Afrika Kulia Ukosefu wa Chakula-Rais Dkt. Samia

DKT Mpango Atoa Wito kwa Serikali za Afrika Kusaidia Wakulima Kuongeza Uzalishaji Chakula

DKT Mpango Atoa Wito kwa Serikali za Afrika Kusaidia Wakulima Kuongeza Uzalishaji Chakula