Mwaimu Akutana na Kuzungumza na Ujumbe wa Balozi wa USA Nchini | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kimataifa

Mwaimu Akutana na Kuzungumza na Ujumbe wa Balozi wa USA Nchini

Septemba 7, 2023 Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mathew Mwaimu (Jaji Mstaafu) amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Balozi wa Marekani nchini Tanzania, ulipotembelea Makao Makuu ya Ofisi za Tume zilizopo mtaa wa Kilimani jijini Dodoma.

Winner Marawiti
By Winner Marawiti
08 Sep 2023
Mwaimu Akutana na Kuzungumza na Ujumbe wa Balozi wa USA Nchini

Ujumbe huo wa watu watatu uliongozwa na Mshauri wa masuala ya Siasa na Uchumi katika Ubalozi huo, Bwana Jonathan Howard aliyeambatana na Bwana Andy Allen  na Bi. Beatrice.

Katika mazungumzo yao Ujumbe huo ulipata fursa ya kuifahamu zaidi Tume na majukumu yake na   Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu.

Pia, katika mazungumzo yao viongozi hao walijadili maeneo mbalimbali ya mashirikiano kwa lengo la kukuza na kulinda haki za binadamu nchini.

Mkurugenzi wa  Malalamiko na Uchunguzi, Bi. Suzana  Pascal aliambatana na Mwenyekiti wa Tume katika mazungumzo hayo.

KOREA KASKAZINI YAWANASA ‘SNIPER’ UKRAINE, YADAI RUSSIA INAWAUA MAJERUHI

KOREA KASKAZINI YAWANASA ‘SNIPER’ UKRAINE, YADAI RUSSIA INAWAUA MAJERUHI

MAREKANI HALI TETE, MOTO WAUA 16 LOS ANGELES, UPEPO WATARAJIWA KUONGEZEKA

MAREKANI HALI TETE, MOTO WAUA 16 LOS ANGELES, UPEPO WATARAJIWA KUONGEZEKA

Maria Sarungi atekwa Kenya wasiojulikana watajwa

Maria Sarungi atekwa Kenya wasiojulikana watajwa

Moto watekeza mitaa, makazi Los Angeles, Marekani

Moto watekeza mitaa, makazi Los Angeles, Marekani