

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mchinga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Salma Rashid Kikwete, ambaye pia ni Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, ameongoza uzinduzi mkubwa wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mchinga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Salma Rashid Kikwete, ambaye pia ni Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, ameongoza uzinduzi mkubwa wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Uzinduzi huo umefanyika katika Kata ya Rutamba, kwenye viwanja vya Mahakama, ambapo Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, alikuwa mgeni rasmi.
Aidha, tukio hilo limepambwa na uwepo wa Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Taifa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye alihudhuria na kutoa baraka zake katika uzinduzi huo.
Katika hatua muhimu ya uzinduzi huo, Mhe. Salma Kikwete alipokea rasmi Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025–2030 kutoka kwa Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa. Vilevile, Waziri Mkuu aliwakabidhi madiwani wote wa Jimbo la Mchinga nakala za Ilani hiyo, akiwataka kushirikiana kwa karibu na Mbunge ajaye katika utekelezaji wake.
Akizungumza wakati wa tukio hilo, Waziri Mkuu Majaliwa aliwahakikishia wananchi wa Mchinga kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao kuhakikisha Ilani ya Uchaguzi inatekelezwa ipasavyo, ili kuboresha maisha ya wananchi na maendeleo ya jimbo hilo.
MTIHANI WA DARASA LA SABA KUFANYIKA SEPTEMBA 10,WADAU WAASWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KIPINDI CHA MITIHANI.
TANESCO YAENDELEA KUBORESHA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUNUNUA VITENDEA KAZI VYA USAFIRI
Doyo Aendelea na Kampeni Muheza, Aahidi Kutatua Changamoto za Wananchi.
MWAGO ATEMA CHECHE AHAIDI MAKUBWA AKIPEWA RIDHAA NA WANANCHI JIMBO LA MBAGALA.
WATEJA WAKUBWA WA HOTELI MOROGORO WAKAMATWA KWA WIZI WA UMEME.
Mavunde: Nitahakikisha Mtumba Inang’aa Kwa Huduma na Maendeleo
Matumizi ya Nishati Safi Kupikia Yapata Msukumo Mpya
WAZIRI MKUU AWATAKA MADEREVA WA SERIKALI KUFANYAKAZI KWA WELEDI
Mbeya Yafurika Kumuaga Mwanahabari Kadala Komba
BRELA YAFANYA KAZI NZURI YA URASIMISHAJI BIASHARA MWANZA