WATEJA WAKUBWA WA HOTELI MOROGORO WAKAMATWA KWA WIZI WA UMEME. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

WATEJA WAKUBWA WA HOTELI MOROGORO WAKAMATWA KWA WIZI WA UMEME.

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewakamata wateja wakubwa wawili mkoani Morogoro ambao ni PH Hotel na Igombe Hotel wakijihusisha na wizi wa umeme ambapo waligundulika kuchepusha nyaya kwenye mita zao aina ya T2 na hivyo kutumia umeme bila kulipa gharama yoyote jambo linalolikosesha Shirika mapato.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
06 Sep 2025
WATEJA WAKUBWA WA HOTELI MOROGORO WAKAMATWA KWA WIZI WA UMEME.

*Ni katika operesheni maalum ya ukaguzi inayofanywa na TANESCO Nchi nzima*

*TANESCO yasisitiza zoezi ni endelevu na kutangaza kiama kwa waolihujumu Shirika*


Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewakamata wateja wakubwa wawili mkoani Morogoro ambao ni PH Hotel na Igombe Hotel wakijihusisha na wizi wa umeme ambapo waligundulika kuchepusha nyaya kwenye mita zao aina ya T2 na hivyo kutumia umeme bila kulipa gharama yoyote jambo linalolikosesha Shirika mapato.

Wateja hao wamekamatwa wiki hii ikiwa ni kati ya wateja 14 waliokamatwa katika operesheni hiyo inayohusisha wataalamu wa mita kutoka Makao Makuu TANESCO wakishirikiana na ofisi ya Mkoa wa TANESCO Morogoro Kaskazini.

Timu hiyo ya ukaguzi ilifika katika maeneo ya Msamvu, Morogoro, ambako hoteli hizo zipo, na kufanikisha kubaini hujuma hizo kwa ushirikiano wa viongozi wa Serikali za Mtaa wa White House pamoja na Jeshi la Polisi.

Aidha, Shirika linaendelea kuimarisha ukaguzi na kushirikiana na vyombo vya dola kuhakikisha hatua kali za kisheria zinachukuliwa dhidi ya wote wanaobainika kujihusisha na vitendo hivyo vinavyolikosesha Shirika mapato.

MTIHANI WA DARASA LA SABA KUFANYIKA SEPTEMBA 10,WADAU WAASWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KIPINDI CHA MITIHANI.

MTIHANI WA DARASA LA SABA KUFANYIKA SEPTEMBA 10,WADAU WAASWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KIPINDI CHA MITIHANI.

Mbeya Yafurika Kumuaga Mwanahabari Kadala Komba

Mbeya Yafurika Kumuaga Mwanahabari Kadala Komba

VIJANA NCHINI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA UFUGAJI SUNGURA KIBIASHARA.

VIJANA NCHINI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA UFUGAJI SUNGURA KIBIASHARA.

MRADI WA TACTIC KUBADILISHA MANDHARI YA JIJI LA DODOMA

MRADI WA TACTIC KUBADILISHA MANDHARI YA JIJI LA DODOMA

SERIKALI KUGHARAMIA MAZISHI YA WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA MGODI NYANDOLWA.

SERIKALI KUGHARAMIA MAZISHI YA WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA MGODI NYANDOLWA.