Mbeya Yafurika Kumuaga Mwanahabari Kadala Komba | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

Mbeya Yafurika Kumuaga Mwanahabari Kadala Komba

MAMIA ya wakazi wa Mbeya wamejitokeza kwenye mazishi ya mwanahabari Kadala Komba (35) aliyefariki jumatatu wiki iliyopita wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma.

Moreen Rojas
By Moreen Rojas
05 Sep 2025
Mbeya Yafurika Kumuaga Mwanahabari Kadala Komba

MAMIA ya wakazi wa Mbeya wamejitokeza kwenye mazishi ya mwanahabari Kadala Komba (35) aliyefariki jumatano tarehe 03 septemba 2025 wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma.

Akihubiri katika ibada iliyofanyika kabla ya mazishi  nyumbani kwao Nzovwe Jijinii Mbeya,  Mchungaji wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) kutoka Bahi mkoa wa Dodoma, Emmanuel Chibwana alisema kuwa kila mwanadamu anatakiwa kuishi maisha ya kumpendeza Mungu.

"Maisha ya duniani yana mwisho kwa kila mtu,mtu anapokufa mwisho wake unakuwa umefika mwisho,lakini baada ya kifo kuna ukaguzi wa mbinguni, ndio maana duniani kuna nyumba za ibada,"alisema 
Alisema kuwa kila mmoja anatakiwa kufanya matendo nema ili apate kuurithi ufalme wa mbinguni.

Alisema kuwa wakati marehemu (Kadala)   akiumwa aliomba aongozwe sala ya toba.

"Aliniomba nimuongoze sala ya toba japo alikuwa ameokoka,baada ya maombi alisema wakati wake wa kuondoka umefika,' alisema

Mchungaji Chibwana alisema kuwa jambo hilo hakulielewa na alianza  kufunga na kuomba kwa ajili yake,lakini kauli yake ilikuwa wakati wake wa kuondoka umefika.

Kadala alizikwa katika makaburi ya Iwambi yaliyopo kwa Jijini Mbeya.

Akisoma wasifu wa marehemu Mwakilishi wa familia Vicent Mapunda, alisema kuwa marehemu alizaliwa Desemba 23,1990 akiwa mtoto wa kwanza kwenye familia ya watoto saba.
Alipata elimu ya msingi na sekondari mkoani Mbeya kabla ya kujiunga na Chuo cha Uandishi wa habari cha Royal.
Alifanya kazi katika maeneo mbalimbali ikiwemo Dodoma Televisheni.
Marehemu ameacha mume na watoto wawili

MTIHANI WA DARASA LA SABA KUFANYIKA SEPTEMBA 10,WADAU WAASWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KIPINDI CHA MITIHANI.

MTIHANI WA DARASA LA SABA KUFANYIKA SEPTEMBA 10,WADAU WAASWA KULINDA AMANI NA UTULIVU KIPINDI CHA MITIHANI.

WATEJA WAKUBWA WA HOTELI MOROGORO WAKAMATWA KWA WIZI WA UMEME.

WATEJA WAKUBWA WA HOTELI MOROGORO WAKAMATWA KWA WIZI WA UMEME.

VIJANA NCHINI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA UFUGAJI SUNGURA KIBIASHARA.

VIJANA NCHINI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA UFUGAJI SUNGURA KIBIASHARA.

MRADI WA TACTIC KUBADILISHA MANDHARI YA JIJI LA DODOMA

MRADI WA TACTIC KUBADILISHA MANDHARI YA JIJI LA DODOMA

SERIKALI KUGHARAMIA MAZISHI YA WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA MGODI NYANDOLWA.

SERIKALI KUGHARAMIA MAZISHI YA WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA MGODI NYANDOLWA.