KAMATI YA SERA YA FEDHA BOT IMETANGAZA UKOMO WA RIBA YA ASILIMIA 6 KWA ROBO YA TATU 2024. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

KAMATI YA SERA YA FEDHA BOT IMETANGAZA UKOMO WA RIBA YA ASILIMIA 6 KWA ROBO YA TATU 2024.

KAMATI ya Sera ya Fedha (MPC) ya Bodi ya Wakurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania, imeamua Riba ya Benki Kuu (CBR) kuendelea kuwa asilimia 6 kwa robo mwaka itakayoishia Septemba 2024 ambapo Uamuzi huu umefikiwa katika kikao cha Kamati kilichofanyika tarehe 3 Julai 2024.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
04 Jul 2024
KAMATI YA SERA YA FEDHA BOT IMETANGAZA UKOMO WA RIBA YA ASILIMIA 6 KWA ROBO YA TATU 2024.

KAMATI ya Sera ya Fedha (MPC) ya Bodi ya Wakurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania, imeamua Riba ya Benki Kuu (CBR) kuendelea kuwa asilimia 6 kwa robo mwaka itakayoishia Septemba 2024 ambapo Uamuzi huu umefikiwa katika kikao cha Kamati kilichofanyika tarehe 3 Julai 2024.

Akisoma taarifa hiyo  leo julai 4 jijini Dar es Salaam Naibu Gavana wa BoT wa sera za uchumi na Fedha, Dk. Yamungu Kayandabila  kwa niaba Gavana wa Benki  Kuu ya Tanzania BoT, Emmanuel Totuba ambaye ni  Mwenyekiti wa Kamati ya Sera ya Fedha amesema uamuzi huo umefanikiwa katika kikao kili chokfanyika jJulai,3 2024  tathimini  ya kamati  kuhusu mwelekeo wa  uchumi na vihatarishi mblimbali inaonesha kwamba utekelezaji wa sera ya fedha kwa kipi cha Januari hadi Juni mwaka huu wamefanikiwa kudhibiti mfumuko wa bei na kubaki chini ya lengo la asilimia 5.
 

"Kamati ya Sera ya Fedha MPC ya Bodi ya Wakurugenzi wa Benki Kuu ya Tanzania imeamua riba  ya Benki Kuu CBR kuendelea kuwa asilimia 6 kwa robo mwaka itakayoisha Septemba mwaka huu,"amesema Dk. Kayandabila.

Amesema  maamuzi ya kamati yamezingatia mtazamo chanya wa uchumi  wa dunia ambapo matarajio ni  kuendelea kupungua kwa mfumuko wa bei katika nchi nyingi kuimarika kwa ukwasi  katika msoko ya fedha duniani na kushuka kwa bei za bidhaa katika soko la dunia.
 

Amesema Kamati hiyo inatarajia uchumi wa ndani kuendelea kukua kwa kasi  na upatikanji wa chakula cha kutosha na kupungua kwa kasi ya kushuka thamani ya shilingi kufuatia ongezeko la mapato ya fedha za kigeni kutokana na shughuli za utalii,pamoja na mauzo ya dhahabu na mazao ya biashara na chakula.


 

"Katika kuthamini mwenendo wa uchumi wa dunia kamati imebaini kuimarika kwa shughuli za kiuchumi katika nchi nyingi kwa robo ya kwanza na ya pili ya mwaka 2024.Mfumuko wa bei unaendelea kupungua na kuimrika kwa ukwasi katika masoko ya fedha duniani na Benki Kuu katika nchi nyingi kuanza kupunguza viwango vya riba ikiwemo bei ya mafuta ghafi licha ya kuongezeka kidogo mwishoni mwa mwezi Juni 2024 huku bei ya dhahabu inaendelea kuwa juu ikiashiria dhahabu kuendelea kutumika kama uwekezaji mbadala katika mazingira y kushuka kwa thamani ya sarafu mbalimbali kutokan na migogoro ya kisiasa duniani,"ameeleza.
 

Amesema kuwa matarajio ni uchumi wa dunia kuendelea kuimarika kwa kipindi kilichobaki cha mwaka 2024/2025 pamoja  na kuwepo kwa hatari ya kuongezeka kwa migogoro ya kisiasa na mizozo ya kibiashara.
 

Aidha Dk. Kayandabala amesema kuhusu mwenendo wa uchumi nchini kamati imeridhishwa na kuendelea na kuimarika kwa shuguli za kiuchumi kutokana na utekelezaji wa sera thabiti na maboresho mbalimbali yenye lengo la kukuza uchumi.
 

TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.

TANESCO YAJA NA KAMPENI MAALUM YA KUHAMASISHA ULIPAJI WA MADENI KWA WATEJA.

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU

ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 107 ZAKAMILISHA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI SIMIYU

MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA

MEATU MTAENDELEA KUPATA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO IKIWEMO NISHATI- DKT.SAMIA

Mifumo Ya Kidijitali Yaleta Mageuzi Makubwa Katika Sekta Ya Umma:Simbachawene

Mifumo Ya Kidijitali Yaleta Mageuzi Makubwa Katika Sekta Ya Umma:Simbachawene

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA.

BEI YA KUJAZA GESI (LPG) KWA MATUMIZI YA KUPIKIA NI HIMILIVU – KAPINGA.