TAZARA YAPONGEZWA KWA KUREJESHA MIUNDOMBINU ILIYOHARIBIKA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

TAZARA YAPONGEZWA KWA KUREJESHA MIUNDOMBINU ILIYOHARIBIKA.

MAMLAKA ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), imepongezwa kwa kasi kikubwa cha urejeshaji wa miundombinu ya reli iliyoharibiwa.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
29 May 2024
TAZARA YAPONGEZWA KWA KUREJESHA MIUNDOMBINU ILIYOHARIBIKA.

MAMLAKA ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), imepongezwa kwa kasi kikubwa cha urejeshaji wa miundombinu ya reli iliyoharibiwa.

Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, katika  ziara yake ya ya kukagua  urejeshwaji wa miundombinu na  huduma za usafiri wa treni ya Tazara kwa kipande cha Ifakara mpaka Lumumwe.

Amesema shughuli hizo zilisimama kupisha urekebishaji wa miundombinu iliyoharibiwa kutokana na mvua zilizonyesha nchini.

"Nitumie nafasi hii kuwapongeza kwa kazi kubwa mliyoifanya, wakati ule nilikuja kwa helikopta miundombinu haikuruhusu kufika hapa ila safari hii nimekuja na kiberenge nimejionea tayari panafikika na kazi kubwa imeshafanyika na changamoto zote mlizosema nimezichukua,”amesema.

Kihenzile ameeleza lengo la ziara hiyo ni  kuona maendeleo yaliyofikiwa na kitu kinachotakiwa kuongezwa nguvu  kuhakikisha usafiri wa reli hiyo ya kihistoria ya Tazara unarejea  kama ilivyokuwa awali kutoka Dar es Salaam hadi Kapiri Mposhi nchini Zambia.

"Pamoja na kufurahia kazi nzuri iliyofanyika hapa, nimeona treni za mizigo zimeanza kupita, ninatoa maelekezo tena kwa Tazara simamieni maeneo yote yaliyobakia kuhakikisha reli yote inarudi katika hali yake huku tukizingatia usalama wa abiria na mizigo ili usafirishaji wa abiria uanze mara moja,” amesisitiza.

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyobya amemshukuru Kihenzile kwa ufuatiliaji wa maendeleo ya urejeshwaji wa miundombinu ya  reli hiyo.

Amesema wilaya hiyo itahakikisha miundombinu inakamilika kwa wakati na huduma zinarejea kwa wananchi.


Akizungumzia maendeleo ya urejeshaji wa miundombinu kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Tazara, Kelvin Kyara ameishukuru Wizara ya Uchukuzi kwa kuendelea kutoa fedha na kusimamia kwa karibu utekelezaji wa ukarabati huo ambao uko mwishoni kukamilika, kurejesha huduma zilizosimama kwa zaidi ya mwezi mmoja


 

TPDC,  ZPDC  ZAENDELEA KUSHIRIKIANA UENDELEZAJI SEKTA YA GESI NCHINI.

TPDC, ZPDC ZAENDELEA KUSHIRIKIANA UENDELEZAJI SEKTA YA GESI NCHINI.

TIB IMEWEKEZA SHILINGI BILIONI 630.3 KATIKA MIRADI YA MAENDELEO.

TIB IMEWEKEZA SHILINGI BILIONI 630.3 KATIKA MIRADI YA MAENDELEO.

Hatua Kali Za Kisheria Kuchukuliwa Kwa Watakaoghushi Cheti Cha Kuhitimu Mafunzo ya JKT.

Hatua Kali Za Kisheria Kuchukuliwa Kwa Watakaoghushi Cheti Cha Kuhitimu Mafunzo ya JKT.

Vituo 94 vimepewa mikopo na NHIF kwa ajili ya kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi.

Vituo 94 vimepewa mikopo na NHIF kwa ajili ya kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi.

UPOTEVU Wa Maji Kwa Mwaka 2021 Ulikuwa Wastani wa Asilimia 64.

UPOTEVU Wa Maji Kwa Mwaka 2021 Ulikuwa Wastani wa Asilimia 64.