![Mwandishi Wetu](https://thedodomapost.co.tz/media/prof/logo.png)
![TAZARA YAPONGEZWA KWA KUREJESHA MIUNDOMBINU ILIYOHARIBIKA.](https://thedodomapost.co.tz/media/news/1716962315.jpg)
MAMLAKA ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), imepongezwa kwa kasi kikubwa cha urejeshaji wa miundombinu ya reli iliyoharibiwa.
MAMLAKA ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), imepongezwa kwa kasi kikubwa cha urejeshaji wa miundombinu ya reli iliyoharibiwa.
Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, katika ziara yake ya ya kukagua urejeshwaji wa miundombinu na huduma za usafiri wa treni ya Tazara kwa kipande cha Ifakara mpaka Lumumwe.
Amesema shughuli hizo zilisimama kupisha urekebishaji wa miundombinu iliyoharibiwa kutokana na mvua zilizonyesha nchini.
"Nitumie nafasi hii kuwapongeza kwa kazi kubwa mliyoifanya, wakati ule nilikuja kwa helikopta miundombinu haikuruhusu kufika hapa ila safari hii nimekuja na kiberenge nimejionea tayari panafikika na kazi kubwa imeshafanyika na changamoto zote mlizosema nimezichukua,”amesema.
Kihenzile ameeleza lengo la ziara hiyo ni kuona maendeleo yaliyofikiwa na kitu kinachotakiwa kuongezwa nguvu kuhakikisha usafiri wa reli hiyo ya kihistoria ya Tazara unarejea kama ilivyokuwa awali kutoka Dar es Salaam hadi Kapiri Mposhi nchini Zambia.
"Pamoja na kufurahia kazi nzuri iliyofanyika hapa, nimeona treni za mizigo zimeanza kupita, ninatoa maelekezo tena kwa Tazara simamieni maeneo yote yaliyobakia kuhakikisha reli yote inarudi katika hali yake huku tukizingatia usalama wa abiria na mizigo ili usafirishaji wa abiria uanze mara moja,” amesisitiza.
Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyobya amemshukuru Kihenzile kwa ufuatiliaji wa maendeleo ya urejeshwaji wa miundombinu ya reli hiyo.
Amesema wilaya hiyo itahakikisha miundombinu inakamilika kwa wakati na huduma zinarejea kwa wananchi.
Akizungumzia maendeleo ya urejeshaji wa miundombinu kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Tazara, Kelvin Kyara ameishukuru Wizara ya Uchukuzi kwa kuendelea kutoa fedha na kusimamia kwa karibu utekelezaji wa ukarabati huo ambao uko mwishoni kukamilika, kurejesha huduma zilizosimama kwa zaidi ya mwezi mmoja
MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO
RAIS DKT SAMIA ATAJWA SHUJAA WA UWEKEZAJI.
DKT.TULIA AMUAPISHA BALOZI KOMBO AMTAKA KUCHAPA KAZI.
RAIS DK.SAMIA awaongoza watanzania maadhimisho ya siku ya mashujaa.
KAGERA, GEITA WATAKIWA KUTUNZA VIFAA VYA UBORESHAJI
DIRA YA TAIFA 2050 NI MAONO YA NCHI SIKU ZA USONI - DKT. BITEKO
WAZIRI BASHE ATANGAZA NEEMA KILIMO CHA UMWAGILIAJI KATAVI.
HISTORIA IMEANDIKWA SGR YAZINDUA SAFARI ZAKE RASMI DAR ES SALAAM-DODOMA.
Vijiji 151 vimebaki nchi nzima kupata huduma ya umeme - Kapinga
WAZIRI MKUU AZINDUA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KIGOMA.