![Sophia kingimali](https://thedodomapost.co.tz/media/prof/logo.png)
![TARURA KUTUMIA TEKNOLOJIA MBADALA KUIMARISHA MTANDAO WA BARABARA.](https://thedodomapost.co.tz/media/news/1716914438.jpg)
Wakala wa barabara Vijijini na mijini (TARURA) inaendelea kutumia Teknolojia mbadala katika kuimarisha mtandao wa barabara ikiwemo ujenzi wa madaraja imara na madhubuti kwa kutumia mawe.
Wakala wa barabara Vijijini na mijini (TARURA) inaendelea kutumia Teknolojia mbadala katika kuimarisha mtandao wa barabara ikiwemo ujenzi wa madaraja imara na madhubuti kwa kutumia mawe.
Akizungumza na waandishi wa habari Mei 27,2024 jijini Dar es salaam katika banda la maonesho la TARURA kwenye mkutano wa 30 wa wahandisi Afrika.Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila amesema Teknolojia ya mawe imeweza kuwa mkombozi kwa kusaidi kupunguza gharama za ujenzi.
“TARURA wanaonesha utaalamu wanafanya ikiwemo ujenzi wa ‘structure’ mbalimbali za kupitishia maji, wanajenga kwa mawe teknolojia hii inasaidia inapunguza gharama za ujenzi lakini pia miundombinu hiyo inadumu kwa muda mrefu,” amesema.
Akizungumzia namna Serikali ilivyojipanga kurejesha miundombinu iliyoharibiwa na mvua zilizoanza kunyesha tangu Oktoba, 2023 na kuendelea hadi sasa, Mativila amebainisha kuwa bado kuna sehemu nyingi mvua zinaendelea kunyesha, miundombinu mingi imeharibika, mvua zilizokuja hazikuwa za kawaida kama miaka mingine hivyo pindi mazingira yatakapokauka urejeshaji utaanza mara moja.
Amesema kufuatia tathimini iliyofanyika kiasi cha Tsh. Bil. 2 zinahitajika kurejeresha miundombinu iliyoharibiwa na mvua na Serikali ipo tayari kutoa fedha hizo
Kwa upande wake Msimamizi wa Teknolojia Mbadala TARURA – Makao Makuu Mhandisi Mshauri Pharels Ngeleja amesema tayari wamejenga madaraja 256 kwa teknolojia ya mawe yaliyogharimu Tsh. Bil. 13.
I “Hii Teknolojia ya mawe tunaitumia pia kujenga barabarani, kuna Km. 26.18 zimekamilika Mkoani Mwanza, Kigoma na Rukwa, pia kwenye barabara zetu zingine tunatumia teknolojia za Ecoroad, Ecozyme na Polymer”.
“Tumejenga barabara ya Sawala Km. 13 Mkoani Iringa, Chamwino - Dodoma pia tunaendelea na hizi teknolojia, Dodoma barabara ya daraja dogo tumekamilisha na Miradi hii ipo maeneo mbalimbali nchi na tunaendelea nayo” amesema Mhandisi Ngereja.
Aidha ameongeza kuwa kupitia kitengo cha mambo ya mazingira wanaendelea pia kufuatilia kwa ukaribu athari za mabadiliko ya tabia nchi ili kujiimarisha zaidi katika ujenzi wa miundombinu yake.
TARURA imeweza kujenga barabara kwa kutumia teknolojia ya Ecoroad, Ecozyme na Polymer katika barabara ya Chamwino Km. 7,Itilima Km. 5, Sawala-Mkonge Km. 10 na Daraja dogo -Dodoma Km.1.
MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO
RAIS DKT SAMIA ATAJWA SHUJAA WA UWEKEZAJI.
DKT.TULIA AMUAPISHA BALOZI KOMBO AMTAKA KUCHAPA KAZI.
RAIS DK.SAMIA awaongoza watanzania maadhimisho ya siku ya mashujaa.
KAGERA, GEITA WATAKIWA KUTUNZA VIFAA VYA UBORESHAJI
DIRA YA TAIFA 2050 NI MAONO YA NCHI SIKU ZA USONI - DKT. BITEKO
WAZIRI BASHE ATANGAZA NEEMA KILIMO CHA UMWAGILIAJI KATAVI.
HISTORIA IMEANDIKWA SGR YAZINDUA SAFARI ZAKE RASMI DAR ES SALAAM-DODOMA.
Vijiji 151 vimebaki nchi nzima kupata huduma ya umeme - Kapinga
WAZIRI MKUU AZINDUA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KIGOMA.