RAIS DKT.SAMIA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WIZARA YA VIWANDA NA WIZARA YA UWEKEZAJI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

RAIS DKT.SAMIA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WIZARA YA VIWANDA NA WIZARA YA UWEKEZAJI.

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewaagiza Waziri wa Viwanda na Biashara Dk.Ashatu Kijaji na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo kuhakikisha mradi wa chuma wa liganga unaanza uzalishaji na malighafi hiyo itumike kwenye viwanda vya hapa nchini.

Sophia kingimali
By Sophia kingimali
09 May 2024
RAIS DKT.SAMIA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WIZARA YA VIWANDA NA WIZARA YA UWEKEZAJI.

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewaagiza Waziri wa Viwanda na Biashara Dk.Ashatu Kijaji na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,  Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo  kuhakikisha mradi  wa chuma wa liganga  unaanza uzalishaji  na malighafi hiyo itumike kwenye viwanda vya hapa nchini.

Akizungumza leo Mei, 9,2024 jijini Dar es Salaam Dk. Samia wakati akizindua kiwanda cha kuunganisha malori na matipa cha Surtun  kilichopo Kisarawe II  Wilaya ya Kigamboni  uliohudhuliwa na viongozi mbalimbali wa Serikali,Taasisi na Dini.

Amesema Malighafi zinazopatikana  katika mradi wa chuma wa liganga  utasaidia  utengenezaji wa vipuri na bidhaa nyingine zinazozalishwa na viwanda vya ndani.

"Mradi huu ni muhimu kwa uchumi  wa viwanda  vya chuma na amewataka mawaziri hawa kuhakikisha  wanapata muwekezaji mzuri atakayechimba chuma hicho na kisha kitumike kwenye viwanda vingine,"amesema Dk.Samia.

Amesema  serikali itaendelea  kujenga  uchumi  wa kisasa  funganishi na jumuishi  na shindani katika  msingi  wa Viwanda,  huduma  za kiuchumi  na miundombinu wezeshi.

Amesema  sekta  ya viwanda inaongoza uzalishaji  na kutoa ajira kwa wananchi jambo ambalo ni muhimu  katika  kukuza kusaidia katika mapambano ta kuondoa umaskini

Dk. Samia  amesema   serikali  imepunguza kodi ya makapuni kutoka asilimia 30 hadi asilimia 10 kwa kipindi  cha miaka  mitano ya mwanzo ili kuchochea  uwekezaji  zaidi kwenye  sekta ya viwanda.

"Kiwanda hiki ni chachu ya ukuaji wa viwanda na sekta nyingine  kwa kuwa  kutumia vioo vinavyozalishwa na kiwanda kingine ambacho zaidi ya asilimia 89 ya malighafi  zake zinapatikana hapa nchini,"amesema.

Pia Dk. Samia  amesema  matumizi  ya bidhaa zinazozalishwa nchini zinapunguza gharama  kwa kampuni zenyewe zinazotengeneza magari na inaongeza manufaa ya uwepo wa kampuni  hiyo kwa uchumi  wa nchi.

Ameongeza  kuwa kiwanda hicho kimetoa ajira  za moja kwa moja 250 na zisizo rasmi  1800 kuongeza  mzunguko wa fedha, mapato ya serikali  na kuhaulisha teknolojia.

Naye Waziri wa Viwanda na Biashara Dk.Ashatu Kijaji,  amesema  uamuzi wa serikali wa kulipa fidia wananchi wanaozunguka mradi wa madini  ya vioo wa Engaruka uliopo Wilaya ya Monduli mkoani Arusha.

Amesema  malighafi zitapatikana katika  mradi huo zitatosheleza kwa zaidi ya asilimia 99 viwanda  vya vioo hapa nchini.

" Mradi huu ni muhimu kwa uchumi  wa viwanda vya vioo na kwamba hatakuwa na haja ya kuagiza malighafi  nje ya nchi,"amesema Dk.  Kijaji.

Amesema  hatua hiyo ya serikali  ni ushindi mkubwa kwa uwekezaji na uzalishaji wa bidhaa za vioo hasa viwanda vilivyopo nchini.

Naye Waziri  wa Nchi Ofisi ya Rais Mpango  na Uwekezaji , Profesa Kitila Mkumbo amesema katika miaka mitatu iliyopita uchumi wa Tanzania  umekua na kuimarika  na ukuaji kwa asilimia sita

Amesema  uchumi  wa Tanzania  umeimarika  kutokana na uwekezaji  uliofanywa  na serikali katika  kilimo na ujenzi  wa miundombinu.

"Sekta ya  viwanda  imekuwa na mchango  chiki ya asilimia 10 katika  miongo mitatu iliyopita lakini  kwa sasa changamoto nyingi  zimetatuliwa na ndio maana  uwekezaji  katika sekta hii unazidi kukua,"amesema Profesa Kitila.

Amesema  kati miradi 526 iliyosajiliwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania kwa mwaka jana, pekee na miradi 237 iliikuwa ni ya uzalishaji  viwandani.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni  ya Surtun  Corporation Limited,Rehmtullah Habib amesemakiwanda hicho  ni  cha kuunganisha  magari aina ya malori na matipa  na kwa siku kinauwezo wa kuzalisha malori 30 na matipa tisa.
 

Amesema hadi sasa wamezalisha magari  150 na wanazalisha aina kuu mbili ambazo trucki na tippa kwaajili ya shughuli. Mbalimbali katika sekta ya ujenzi na madini.

" kiwanda hiki kimeajiri watu 250 na ajira zisizo rasmi 1800 wakati tunaanza kuuza magari walikuwa 20 tangu kiwanda kianze ajira  zimeongeza,"amesema Habib.

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO

MHANDISI SEFF AMTAKA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KASULU-KABANGA-MUYAMA KUMALIZA KAZI KWA WAKATI

MHANDISI SEFF AMTAKA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KASULU-KABANGA-MUYAMA KUMALIZA KAZI KWA WAKATI

Serikali ya Tanzania kuendelea kushirikiana na Serikali ya Zanzibar

Serikali ya Tanzania kuendelea kushirikiana na Serikali ya Zanzibar

RC MTWARA AIPONGEZA WIZARA YA FEDHA KWA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI.

RC MTWARA AIPONGEZA WIZARA YA FEDHA KWA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI.