WATU 16 wamekamatwa na Madawa ya kulevya. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

WATU 16 wamekamatwa na Madawa ya kulevya.

Mamlaka ya kuthibiti na kupambana na madawa ya kulevya imewakamata watu 16 waliohusika na kilimo cha madawa ya kulevya aina ya bangi.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
03 May 2024
WATU 16 wamekamatwa na Madawa ya kulevya.

Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na madawa ya kulevya imewakamata watu 16 waliohusika na kilimo cha madawa ya kulevya aina ya bangi.

Hayo yameelezwa na Kamishna msaidizi kanda ya kati Mzee Kasuwi wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu taarifa ya operesheni ya dawa za kulevya kanda ya kati Dodoma na kukabidhi silaha mbili kwa RPC Dodoma zilizopatikana kwenye operesheni tarehe 24 hadi 28 Aprili,2024.

Aidha amesema kuwa katika operesheni hiyo walifanikiwa kukamata silaha mbili za moto aina ya gobore  zilizokuwa zinamilikiwa na Hamisi chambo mzigua mwenye umri wa miaka 46 pamoja na Abdilah Juma Mgogo  mwenye umri wa miaka 45 wakazi wa kata ya segera ambao walikuwa wanamiliki  kinyume cha sheria na kwamba zilikuwa zinatumiwa na watuhumiwa kulinda mashamba ya bangi."Tarehe 24 hadi 28 Aprili 2024,mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya kanda ya kati Dodoma imefanya operesheni katika maeneo ya wilaya ya Chamwino na Dodoma mjini na kufanikiwa kuteketeza ekari 9.5 za mashamba ya bangi,kukamata jumla ya kilogramu 156.23 za bangi na misokoto 127 ya bangi,watu 16 wamekamatwa kuhusika na dawa hizo na watafikishwa mahakamani baada ya taratibu za kisheria kukamilika" Ameongeza Kasuwi.

Amesema kuwa kwa niaba ya kamishna Jenerali wa mamlaka ya kudhibibiti na kupambana na dawa za kulevya anakabidhi silaha hizo kwa kamanda wa polisi wa Mkoa wa Dodoma kwa hatua zaidi za kisheria.

Aidha amewaomba wananchi kuendelea kutoa taarifa za watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya kwa kupiga simu kupitia namba yao ya bure 199.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa  Dodoma(RPC) Theopista Mallya ameishukuru Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya kwa kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi kutokomeza uhalifu na kutoa rai kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwa kumiliki silaha hatarishi na badala yake kufuata sheria za nchi na taratibu zake kwani Jeshi la polisi lipo na litaendelea kutokomeza matumizi mabaya ya dawa za kulevya.

“Kuna maeneo ambayo tumeelekezwa na tutaenda kuwakamata sababu hawa watu wanalinda haya mashamba kwa kutumia silaha za moto kwa hiyo wananchi waone uhatari uliopo wa hawa watu ambao wanajihusisha dawa ya kulevya,”amesema.

Amewataka wananchi kuwafichua watu wanaojihusisha na biashara hizo kwani wamekuwa hatari kwa jamii na kwa taifa kwa ujumla.

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO

MHANDISI SEFF AMTAKA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KASULU-KABANGA-MUYAMA KUMALIZA KAZI KWA WAKATI

MHANDISI SEFF AMTAKA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KASULU-KABANGA-MUYAMA KUMALIZA KAZI KWA WAKATI

Serikali ya Tanzania kuendelea kushirikiana na Serikali ya Zanzibar

Serikali ya Tanzania kuendelea kushirikiana na Serikali ya Zanzibar

RC MTWARA AIPONGEZA WIZARA YA FEDHA KWA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI.

RC MTWARA AIPONGEZA WIZARA YA FEDHA KWA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI.