MHAGAMA: wananchi changamkieni fursa za uwekezaji Nchini | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

MHAGAMA: wananchi changamkieni fursa za uwekezaji Nchini

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama ametoa shime kwa Baraza la Uwekezaji wa Wananchi Kiuchumi kwa kushirikiana na sekta binafsi na wadau mbalimbali kutambua mawanda makubwa ya uwekezaji yaliyo katika nchi yetu.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
28 Apr 2024
MHAGAMA: wananchi changamkieni fursa za uwekezaji  Nchini

Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza katika Kongamano la Nne la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya kimkakati na uwekezaji lilofanyika leo tarehe 27 Aprili, 2024 katika ukumbi wa Benki kuu ya Tanzania (BOT) Jijini Dar es salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama(kulia) akiteta jambo na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bi. Beng'i Issa (kushoto) wakati wa Kongamano la Nne la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati na uwekezaji linalofanyika katika ukumbi wa BOT Jijini Dar es Salaam.
 

Waziri Mhagama amesema kuwa sekta binafsi na wadau mbalimbali waendelee kutoa mapendekezo kwenye fursa mbalimbali zinazojitokeza za kiuchumi ili kuwezesha utekelezaji wa miradi ya kiuchumi kufikia malengo yaliyopo.

Ameongeza kusema wananchi wa Tanzania wako tayari wakiongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameonesha kwa vitendo kwamba yuko tayari hivyo ni vyema kumuunga mkono kwa kufanya kazi ili kujenga uchumi wa Taifa.

Aidha jukwaa hilo litasaidia kujenga uelewa wa pamoja juu ya mafanikio yaliyopatikana na katika uwekezaji na ustawi wake wa kiuchumi.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji (NEEC) Bi. Beng'i Issa akitoa taarifa fupi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama aliposhiriki Kongamano la Nne la Kitaifa la Ushiriki wa watanzania katika Miradi ya kimkakati na uwekezaji.

Waziri aliongezea dhana ya kongamano hilo lenye  kauli Mbiu ya “Wekeza Tanzania kuongeza thamani ya ziada” linatumika kujenga uchumi imara ambao umeshirikisha Watanzania wengi.

“Na itatutengenezea mazingira mazuri ya biashara ambayo yatachochea wananchi wengi katika uwekezaji na ushiriki wao katika kujenga uchumi,"alisema Waziri Mhagama

Matukio katika picha baadhi ya Washiriki waliohudhuria Kongamano la Nne la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati na uwekezaji linalofanyika katika ukumbi wa BOT Jijini Dar es Salaam  wakifuatilia uwasilishaji wa taarifa mbalimbali.
 

Baraza la Uwekezaji wa Wananchi Kiuchumi limeingia makubaliano na taasisi ya serikali inayosimamia manunuzi ya umma, katika moja ya kipengele katika sheria ya manunuzi ya umma kinachosisitiza kila asilimia 30 ya manunuzi ya umma ya kila mradi yaende kwa vijana, wanawake wazee na watu wenye ulemavu ambayo ni sehemu ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

Matukio tofauti katika picha ya baadhi ya wawasilishaji wa mada mbalimbali wakizungumza wakati wa Kongamano la Nne la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati na uwekezaji linalofanyika katika ukumbi wa BOT Jijini Dar es Salaam

Kwa upande wake Bibi, Beng’i Issa Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi wa Kiuchumi (NEEC) amesema moja ya mambo wanayosimamia ni kuangalia kampuni zinazopata kazi kwenye miradi ya kiuchumi na bidhaa zinazouzwa katika miradi hiyo  zinatoka nchini.

Aidha kwenye ajira Baraza la Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi linaangalia ajira za moja kwa moja na ajira ambazo sio za moja kwa moja katika uhaulishaji wa teknolojia kwa kusimamia teknolojia nchini na mipango ya kutoa mafunzo ya kuhaulisha inafanyika

Akizungumzia kuhusu kongamano amesema kongamano hilo la Nne limelenga katika kujenga uelewa wa pamoja kuhusu ushiriki wa watanzania katika miradi ya kimkakati na uwekezaji unaofanyika hapa nchini pamoja na kushirikishana mafanikio na changamoto zilizopo katika ushiriki wa watanzania katika uwekezaji.

Matukio tofauti katika picha ya baadhi ya wawasilishaji wa mada mbalimbali wakizungumza wakati wa Kongamano la Nne la Kitaifa la Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati na uwekezaji linalofanyika katika ukumbi wa BOT Jijini Dar es Salaam


 

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO

MHANDISI SEFF AMTAKA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KASULU-KABANGA-MUYAMA KUMALIZA KAZI KWA WAKATI

MHANDISI SEFF AMTAKA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KASULU-KABANGA-MUYAMA KUMALIZA KAZI KWA WAKATI

Serikali ya Tanzania kuendelea kushirikiana na Serikali ya Zanzibar

Serikali ya Tanzania kuendelea kushirikiana na Serikali ya Zanzibar

RC MTWARA AIPONGEZA WIZARA YA FEDHA KWA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI.

RC MTWARA AIPONGEZA WIZARA YA FEDHA KWA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI.