

Umoja wa wanawake nchini(UWT) umedhamiria kwa vitendo kuhakikisha unatekeleza dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha inamtua kuni mwanamke kichwani kwa kuhakikisha inazalisha nishati mbadala kwa ajili ya kupikia.
Umoja wa wanawake nchini(UWT) umedhamiria kwa vitendo kuhakikisha unatekeleza dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha inamtua kuni mwanamke kichwani kwa kuhakikisha inazalisha nishati mbadala kwa ajili ya kupikia.
Hayo yamesemwa leo March 28,2024 Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa UWT Joketi Mwegelo wakati akipokea ugeni wa wawekezaji kutoka china katika jimbo la Changzho walioletwa nchini na kampuni ya Amec Group kwa kushirikiana na Canopus Energy Solution lengo likiwa kujadiliana na kuangalia wanaweza kushirikiana kwenye maeneo gani katika uwekezaji.
Amesema ugeni huo umekuja kwa wakati muafaka kwani Chama Cha Mapinduzi CCM kimetoa maelekezo kwa jumuiya zake kuweza kujitegemea kiuchumi.
"Chama kilitoa maelekezo kwa Jumuiya zake kuweza kujitegemea hivyo sisi kama UWT tumekuwa tukikimbizana ili kuhakikisha tunapata wawekezaji ili kuendeleza maeneo yetu nchi nzima",Amesema Mwegelo.
Amesema UWT wanampango wa kuzalisha mkaa mbadala unaotokana na mavumbi ya maakaa ya mawe hivyo kutokana na wawekezaji hao kujikita zaidi kwenye teknolojia itawasaidia kutumia teknolijia hiyo katika uzalishaji.
Amesema katika miradi yote watahakikisha wanajielekeza katika kumuwezesha mwanamke hivyo chochote watakachoanzisha kitamgusa mwanamke moja kwa moja ili kuhakikisha wanamuinua kiuchumi.
"Tunajivunia kuwa na kundi kubwa la wanawake hivyo tunauwezo wa kuwafikia wanawake wote nchini hivyo tukijua hawa wawekezaji watakuja kuwekeza kwenye maeneo gani tutahakikisha tunawafikia wanawake husika kwani",Amesema.
Sambamba na hayo Mwegelo ametoa rai kwa wanawake nchini kuungana,kuwezeshana na kujengana kiuchumi kwani kwa kufanya hivyo wanaweza kufanya mambo makubwa katika uchumi wao na Taifa kwa jumla.
Ameongeza kuwa kwa sasa wapo kwenye usajili wa wanawake kote nchini kwenye mfumo wao hivyo hiyo itawasaidia kuendelea kuwaunganisha wanawake ili hata sera za nchi zilizowekwa ziweze kuwasaidia.
Kwa upande wake
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege