RC CHALAMILA AZINDUA PROGRAMU YA KONEKT UMEME, PIKA KWA UMEME | The Dodoma Post
The Dodoma Post Nishati

RC CHALAMILA AZINDUA PROGRAMU YA KONEKT UMEME, PIKA KWA UMEME

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Octoba 09,2025 amezindua programu ya Konekt Umeme, Pika kwa Umeme iliyobuniwa na TANESCO katika viwanja vya Mwembe yanga wilaya ya Temeke.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
09 Oct 2025
RC CHALAMILA AZINDUA PROGRAMU YA KONEKT UMEME,  PIKA KWA UMEME

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Octoba 09,2025 amezindua programu ya Konekt Umeme, Pika kwa Umeme iliyobuniwa na TANESCO katika viwanja vya Mwembe yanga wilaya ya Temeke.

Programu ya Konekt Umeme, pika kwa umeme ni gharama nafuu, inaufanisi mkubwa, pia  umeme unaotumika ni kidogo sana ukilinganisha na nishati zingine.

RC Chalamila amepongeza Wizara ya Nishati, na TANESCO na wadau wote wa maendeleo kwa kuja na wazo hili bunifu lenye lengo la kuongeza upatikanaji wa Nishati safi ya kupikia kwa Watanzania. "Mpango huu ni mwanzo wa zama mpya katika historia ya huduma za umeme nchini unaounga mkono juhudi ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu katika matumizi ya nishati safi".

Kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya umeme kupikia unaifanya jamii ya kitanzania kwenda kwenye viwango bora vya maisha.

Vilevile RC Chalamila amesema ni ukweli usiopingika umeme ni hitaji muhimu kwa maendeleo ya uchumi wa nchi lakini maendeleo ya mtu mmoja mmoja.

Aidha kwa upande wa Mtendaji mkuu wa TANESCO Bw Lazaro Twange amesema Tanzania kupitia wizara ya Nishati, TANESCO  imetangaza rasmi mpango wa kitaifa wa Nishati (Energy Compact) wenye lengo la kuunganisha wateja milioni 8.5 ifikapo 2030 sawa na wateja milioni 1.7 wapya kila mwaka hivyo uzinduzi wa programu ya Konekt Umeme, Pika kwa umeme umefanyika muda muafaka.

Sanjari na hilo amesema  mpango huu unatoa fursa kwa mteja kupewa jiko wakati wa kuunganishiwa umeme kisha analipa kidogo kidogo kupitia mfumo wa token hivyo familia nyingi sasa zitaweza kupika kwa ufanisi na kwa gharama nafuu.

Mwisho RC Chalamila amegawa majiko ya Nishati safi ya umeme kwa wananchi mbalimbali na kuwataka kuwa mabalozi kwa jamii ya kitanzania.

 

 

 

 

 

TANESCO YATEKELEZA KWA MAFANIKIO PROGRAMU YA “KONEKT UMEME, PIKA KWA UMEME” NCHI NZIMA

TANESCO YATEKELEZA KWA MAFANIKIO PROGRAMU YA “KONEKT UMEME, PIKA KWA UMEME” NCHI NZIMA

TANESCO YAPATA TUZO YA UTOAJI HUDUMA BORA KWA WATEJA 2025.

TANESCO YAPATA TUZO YA UTOAJI HUDUMA BORA KWA WATEJA 2025.

TANESCO YAZINDUA KAMPENI KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI.

TANESCO YAZINDUA KAMPENI KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI.

TANESCO YAKUTANA NA WADAU MOROGORO KUJADILI MIKAKATI YA KUTUNZA VYANZO VYA MAJI BWAWA LA JNHPP

TANESCO YAKUTANA NA WADAU MOROGORO KUJADILI MIKAKATI YA KUTUNZA VYANZO VYA MAJI BWAWA LA JNHPP

UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE WAIMARIKA

UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE WAIMARIKA