WANANCHI WAAHIDI KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29 | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

WANANCHI WAAHIDI KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

Wananchi wenye haki ya kupigakura katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 wamehamasishwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 ili kuchagua Viongozi wanaoweza kuwaletea maendeleo na kutimiza wajibu wao wa Kikatiba na kidemokrasia.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
08 Oct 2025
WANANCHI WAAHIDI KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

Wananchi wenye haki ya kupigakura katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 wamehamasishwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 ili kuchagua Viongozi wanaoweza kuwaletea maendeleo na kutimiza wajibu wao wa Kikatiba na kidemokrasia.

Wananchi hao pia akiwemo Mwanahuba Jumbe Ramadhani wamesisitiza umuhimu wa kutii sheria na Miongozo ya uchaguzi, akisema ifikapo Oktoba 29, 2025 mara baada ya zoezi la kupiga kura ni muhimu kila mmoja akarejea nyumbani na kuendelea na shughuli zake badala ya kutii wito unaotolewa na baadhi ya wanasiasa wa kulinda kura kwenye Vituo, kazi ambayo ni ya mawakala wa vyama vya siasa na tume huru ya Taifa ya uchaguzi.

Richard Alphonce na Bw. Abdallah Ismail Haruna, wakazi wa Dar Es Salaam wakisisitiza kuwa kura ni haki ya kimsingi, wamebainisha kuwa mabalozi wazuri wa uchaguzi kwa kuhamasisha Vijana wenzao kupiga kura na kujitokeza kwa wingi kwani kura ndio njia pekee ya kidemokrasia ya kuweza kumchagua Kiongozi sahihi pamoja na kuwawajibisha wale walioko madarakani na walioshindwa kutimiza ahadi na matarajio ya wananchi.

Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha

Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha

HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA

HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO

Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya  VSOMO ya VETA

Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya VSOMO ya VETA

WENYE ULEMAVU WAHAMASISHA KUJITOKEZA KUWACHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTETEA MASLAHI YAO

WENYE ULEMAVU WAHAMASISHA KUJITOKEZA KUWACHAGUA VIONGOZI WANAOWEZA KUTETEA MASLAHI YAO