SHUJAA ALIYEPIGANA VITA ASISITIZA AMANI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

SHUJAA ALIYEPIGANA VITA ASISITIZA AMANI.

Mwakilishi wa mashujaa waliopigana vita vya kagera Balozi Brigedia Jenerali Francis Benard Mndolwa amesema anajivunia kuwa mmoja wa wapigania uhuru na kuwa mzalendo Kwa nchi yake na amewasihi wafanyakazi wote kuwa wazalendo.

Moreen Rojas, Dodoma
By Moreen Rojas, Dodoma
25 Jul 2025
SHUJAA ALIYEPIGANA VITA ASISITIZA AMANI.

Ameyasema hayo wakati wa Maadhimisho ya siku ya Kumbukumbu ya mashujaa tarehe 25 julai, 2025 katika uwanja wa mashujaa mji wa Serikali   Mtumba jijini Dodoma ambapo mgeni Rasmi alikuwa ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

"Hata nyinyi waandishi wa habari nawasihi kuwa wazalendo kwa kuandika habari zinakazowainua na kuwaheshimisha hivyo waandishi wa habari wote wanapaswa kuwa wazalendo kwani nchi hii inahitaji msaada wa Kila mmoja wetu"

Aidha amesema ili tuendelee kuwa na amani ni lazima kutanguliza uzalendo Kwani nchi nyingi zimeingia kwenye matatizo kwa kushindwa kulinda amani lakini Kwa hapa Tanzania Waasisi wa Taifa hili Mwalimu Julius Nyerere na Karume wamefanya kazi kubwa sana.

"Tusiwe na mwenendo wa upinzani wa Dunia Kama warusi na china wanajaribu wakipambana lakini sisi hatuyataki hayo Umoja wetu Tanzania Bara na Tanzania Visiwani lazma tushirikiane kuilinda amani yetu"

Kwa upande wake mkazi wa Mtumba Bi.Leila Juma amesema anafurahia kuwa sehemu ya Kumbukumbu hii muhimu ya kuwaenzi mashujaa waliopigana Kwa ajili ya Taifa lao

"Nafurahi kuwa sehemu ya historia hii kiukweli nawapongeza mashujaa wetu kwani bila wao tusingekuwa hapa hivyo niwasihi watanzania wenzangu tuendelee kuilinda amani ya nchi yetu"Amesisitiza Bi.Leila

WAZIRI MKUYA AZIPONGEZA DIB, BoT KUSHUGHULIKIA UFILISI WA FBME

WAZIRI MKUYA AZIPONGEZA DIB, BoT KUSHUGHULIKIA UFILISI WA FBME

DK.MPANGO AWATAKA WANANCHI KUTUMIA MIFUMO YA KIDIGITALI KUFANYA MALIPO,AIPONGEZA BoT KUZINDUA MFUMO MKUU JUMUISHI WA KIBENKI.

DK.MPANGO AWATAKA WANANCHI KUTUMIA MIFUMO YA KIDIGITALI KUFANYA MALIPO,AIPONGEZA BoT KUZINDUA MFUMO MKUU JUMUISHI WA KIBENKI.

TBC KUAZIMISHA MIAKA 26 YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA HAYATI MWALIMU NYERERE KWA KUENDESHA MASHINDANO YA INSHA KWA WANAFUNZI.

TBC KUAZIMISHA MIAKA 26 YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA HAYATI MWALIMU NYERERE KWA KUENDESHA MASHINDANO YA INSHA KWA WANAFUNZI.

GAVANA TUTUBA: BENKI KUU ZIWE WASHIRIKA WA MAGEUZI YA KIUCHUMI

GAVANA TUTUBA: BENKI KUU ZIWE WASHIRIKA WA MAGEUZI YA KIUCHUMI

Rais Samia Azindua Dira Ya Taifa Ya Maendeleo 2050, Asisitiza Utekelezaji Wa Vitendo Na Upimaji Wa Matokeo

Rais Samia Azindua Dira Ya Taifa Ya Maendeleo 2050, Asisitiza Utekelezaji Wa Vitendo Na Upimaji Wa Matokeo