

Kesi inayomhusu rapa maarufu A$AP Rocky imeendelea kuibua maswali baada ya tukio la kipekee kutokea mahakamani. Katika kusikiliza kwa kesi ya shambulio mapema jana, A$AP Rocky alijitokeza kumzuia rafiki yake, A$AP Twelvyy, asijibu swali lililoulizwa na mahakama, jambo lililosababisha hali ya kutatanisha.
Waendesha mashtaka walimhoji Twelvyy kuhusu picha ya kitanda cha Rocky kilichoandikwa neno "AWGE", wakitaka kujua maana yake. Kabla Twelvyy hajatoa majibu, Rocky alikurupuka kwa kupaza sauti akisema, "Usiseme!" Hali hiyo ilisababisha hali ya mshikamano, huku Twelvyy akijibu kwa upole, "Inamaanisha AWGE."
Hata hivyo, mwendesha mashtaka alikasirishwa na ukimya wa Twelvyy, na aliiomba mahakama iamulie kumlazimisha kutoa majibu ya moja kwa moja. Hata hivyo, Twelvyy alikataa kusema chochote zaidi kuhusu maana ya herufi hizo nne. Wakili wa A$AP Rocky, Joe Tacopina, alijitokeza kuomba mazungumzo ya faragha na jaji ili kuzuia kuendelea kwa uchunguzi huu.
Mwisho wa siku, Twelvyy alikataa kufichua siri hiyo ya "AWGE", inayodaiwa kuwa ni shirika la ubunifu lilioanzishwa na Rocky mwaka 2014. Kwa mujibu wa taarifa, kanuni kuu ya AWGE ni ‘Kamwe usifichue maana ya AWGE’.
A$AP Rocky, ambaye anahusishwa na mashtaka mawili ya uhalifu, anadaiwa kumshambulia kwa risasi rafiki yake wa zamani na mshirika wa kundi la muziki la ASAP Mob.
MKURUGENZI WA MASOKO TTB AELEZA FURSA INAYOWEZA KUPATA TANZANIA KUTOKA JAPAN KATIKA ELIMU YA UTALII NA UHIFADHI
MENEJIMENTI YA NCAA YAPATA MAFUNZO YA KUBORESHA UTENDAJI KAZI
BALOZI LUVANDA AONGOZA UJUMBE WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAKALA WA UTALII NCHINI JAPAN
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
BEI YA MADINI YA DHAHABU IMEPANDA HADI DOLA ZA MAREKANI 2,655.80
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
TUME YATAKA WANANCHI KUTAZAMA DAFTARI LA AWALI,KUHAKIKI TAARIFA ZAO
TUTAENDELEA KUINADI TANZANIA KWA NGUVU ZOTE EXPO 2025 JAPAN- MWAMWAJA.