

Mtangazaji maarufu wa kituo cha redio cha EFM, #DrKumbuka, ametoa kauli kali kuhusu kuvunjika kwa ndoa ya aliyekuwa msemaji wa klabu ya Simba, #HajiManara, na mrembo wake #Zaiylissa.
Akizungumza kwenye kipindi chake, #DrKumbuka amesema kuwa, “Mwanaume kurogwa kwenye mapenzi ni kitu cha kawaida kabisa. Wengine tunarogwa kimapenzi na hatujui.”
Kauli hiyo imekuja baada ya taarifa kusambaa mtandaoni zikionesha kuwa ndoa ya Manara na Zaiylissa imevunjika rasmi, huku wawili hao wakidaiwa kutoleana vitu vya ndani na kuacha nyumba ikiwa tupu.
Katika ushauri wake kwa Haji Manara, Dr Kumbuka alieleza kuwa endapo atahitaji kufunga ndoa tena, ni muhimu kutafuta mwanamke aliyekomaa kiakili, kihisia, na ambaye wanalingana kiumri.
“Ndoa si picha za Instagram, ni maisha halisi. Tafuta mtu ambaye amemaliza kila kitu – siyo bado yupo kwenye kipindi cha kujaribu maisha.” – aliongeza.
Hadi sasa, Manara hajatoa kauli rasmi kuhusu kilichojiri, lakini mashabiki wake mitandaoni wameendelea kumshauri apumzike kwanza kabla ya kurudi tena kwenye anga za mapenzi.
Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum
DIB YAHIMIZA WANANCHI KUDAI FIDIA ZAO KUTOKA BENKI ZILIZOFILISIKA
USHIRIKI WA TAWA KATIKA MAONESHO YA 49 YA BIASHARA YA KIMATAIFA
DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA
BoT YAWATAKA TAMFI NA TAMIU KUBORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA NDOGO ZA FEDHA.
Aliyeongoza kura maoni Vunjo 2020, kumkabili tena Dkt. Kimei
Maiko Salali achukua fomu ya ubunge Jimbo la Mpwapwa
Serikali kufanya mageuzi ya kimtazamo katika nafasi za uongozi kwa wanawake
Dkt.Tulia Aweka Jiwe La Msingi Ujenzi wa Shule ya Wavulana Bunge.
Mavunde Akabidhi Jengo la kupumzikia Wananchi Hospitali ya Rufaa ya Dodoma