

Jamii ya Wahadzabe wanaopatikana kwenye eneo la Mang'ola Wilayani Karatu Mkoani Arusha wameahidi kujitokeza kwa wingi kutimiza haki yao ya Kikatiba ya kuchagua Viongozi katika uchaguzi Mkuu wa Jumatano ijayo Oktoba 29, 2025.
Jamii ya Wahadzabe wanaopatikana kwenye eneo la Mang'ola Wilayani Karatu Mkoani Arusha wameahidi kujitokeza kwa wingi kutimiza haki yao ya Kikatiba ya kuchagua Viongozi katika uchaguzi Mkuu wa Jumatano ijayo Oktoba 29, 2025.
Wananchi hao wametoa kauli hiyo leo Jumatano Oktoba 22, 2025, wakiishukuru serikali pia kwa kuwakumbuka na kuwajumuisha katika zoezi hilo la Kikatiba licha ya kuishi kwao maeneo ya pembezoni na Jamii nyingine, wakisema wanatarajia kushiriki kwenye uchaguzi huo kikamilifu ili kuwachagua Viongozi wanaoweza kuwaletea maendeleo.
"Kwaniaba ya wenzangu Jamii ya Wahadzabe niwahakikishie kuwa tutaenda kupiga kura tarehe 29 na tutachagua Viongozi watakaoenda kutuangalia sisi kwa ujumla Wahadzabe wote ili tufanikiwe kimaendeleo kwasababu sisi tunaishi porini na hatujui mengi yanayoendelea kwahiyo tutawachagua wanaoweza kutuletea maendeleo huku." Amesema mmoja wa wananchi wa Jamii hiyo.
Kwa upande wao Ruben Mathayo, Mwenyekiti wa Jamii ya Wahadzabe Tanzania na Mariam Anyanyire, Mhamasishaji ndani ya jamii hiyo, wameeleza kuwa muamko ni mkubwa kwa jamii hiyo kuelekea uchaguzi Mkuu wakiahidi kuwa kila mwenye haki na sifa ya kupiga kura atajitokeza siku hiyo kuwachagua Viongozi wanaowataka.
NDANI YA MIAKA MINNE YA DKT. SAMIA MADARAKANI UCHUMI UMEPAA- PROF. ASSAD
TANESCO YATEKELEZA KWA MAFANIKIO PROGRAMU YA “KONEKT UMEME, PIKA KWA UMEME” NCHI NZIMA
Viongozi wa dini Kaskazini wahimiza amani kuelekea Uchaguzi Mkuu
AMANI NDIYO HIFADHI YA MWANADAMU, TUILINDE- VIONGOZI WA DINI
HATUTOWAACHA SALAMA WANAOPANGA KUVURUGA UCHAGUZI MKUU- RC SENDIGA
PADRI NIKATA ALIJIPOTEZA KUTOKANA NA MSONGO WA MAWAZO NA KUACHWA NA MPENZI WAKE- POLISI
WANNE JELA MIAKA SABA KWA JARIBIO LA KUMTEKA MFANYABIASHARA
CHALAMILA: WATAKAOJIZIMA DATA OKTOBA 29, TUTAWAFANYA NETWORK ZISOME
JWTZ NA POLISI MOROGORO WAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUJIIMARISHA KATIKA ULINZI NA USALAMA
RC MAKALLA AWAHAKIKISHIA USALAMA WAZEE WA MKOA WA ARUSHA SIKU YA UPIGAJI KURA OKTOBA 29.