Wazee wa Yanga Dodoma watoa msimamo wataka Karia aombe radhi | The Dodoma Post
The Dodoma Post Michezo

Wazee wa Yanga Dodoma watoa msimamo wataka Karia aombe radhi

Uongozi wa wazee wa Yanga na uongozi wa mkoa wa Dodoma wamemtaka Rais wa shirikisho wa mpira wa miguu Tanzania Wallace Karia kuomba radhi kwa timu yao kufuatia kauli waliyoiita ya kuwafokea

Moreen Rojas
By Moreen Rojas
18 Mar 2025
Wazee wa Yanga Dodoma watoa msimamo wataka Karia aombe radhi

Akizungumza Kwa niaba ya Wazee wengine Abdalah Mtosa  amesema hawaoni sababu ya kurudia mchezo ambao tayari ulipangwa kisheria na kuahirishwa bila utaratibu siku ya Machi 8,2025

Mzee Mtosa amesema siku pekee ambayo ilikuwa halali kwa mchezo huo kuchezwa tayari imepita na ilikuwa inatosha kabisa kuwakutanisha watani kwani maandalizi yote yalikuwa yameshakamilika.

"Nimepokea kwa masikitiko makubwa sana Kwa kuahirishwa kwa mchezo wa Machi 8 mwaka huu, kwahiyo na sisi hatuna imani na karia kwani tunajua wazi hana mapenzi ya dhati na yanga

hivyo niwaombe viongozi wa juu kutokuruhusu mechi kufanyika tena Kwa wakati mwingine kama ni faini tuko tayari kulipa lakini sio kurudia mechi na simba". amesema Mtosa

Naye Mzee Bodar Awadhi  amesema mechi kuahirishwa imefanya kutokea mkanganyiko na sintofahamu kwa mashabiki wa soka na hivyo kundi  kubwa halitaki tena hiyo mechi.

Kauli ya kutokuwa na imani tena na Rais Karia imekuja mara baada ya kuahirishwa Kwa dabi ya karikakoo na Kutokana na kauli aliyoitoa ambayo wameita kauli ya kuwafokea.


"Sisi msimamo wetu ni kutokurudia mechi kwanza RAIS wa TFF ametudhalilisha wanayanga na kama ameshindwa mpira arudi kwenye taaluma yake kwani tunaijua"

Kwa upande wake Mratibu wa yanga Dodoma Elisha Ngwando amesema Karia aombe Radhi kwa Wanachama  wa Yanga na wanamichezo kwa alichokifanya na kauli aliyoitoa.

"Watu wametumia gharama kubwa wengine  wamelipia matangazo kwa ajili ya mechi hiyo"

ALLY KAMWE mikononi mwa Polisi, yataja chanzo

ALLY KAMWE mikononi mwa Polisi, yataja chanzo

Kylian Mbappé: Mapambano ya Kifundo cha Mguu na Tumaini la Ushindi

Kylian Mbappé: Mapambano ya Kifundo cha Mguu na Tumaini la Ushindi

MCHEZO WA RIADHA KINARA, KUPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA

MCHEZO WA RIADHA KINARA, KUPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA

AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.

AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.

MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.

MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.