SERIKALI imewahimiza wananchi kutumia msimu wa sikukuu na likizo kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili kujifunza, kuburudika na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma jana, Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii you Tanzania (TTB) Ernest Mwamwaja alisema Tanzania imejaliwa kuwa na vivutio vya kipekee ambavyo vinapaswa kuthaminiwa na Watanzania wenyewe.
“Msimu huu wa sikukuu ni fursa muhimu kwa wananchi kutembelea vivutio vilivyopo nchini ili kujivunia urithi wetu wa asili na kiutamaduni,”alisema
Aliongeza kuwa:”Tulizindua kampeni maalumu ya kuhamasisha utalii wa ndani kati msimu huu wa sikukuu ijulikanayo kama “Funga mwaka kijanja talii “ ambayo inalenga kuwahamasisha watanzania wa rika zote kushiriki katika shughuli za utalii ambayo itakoma ifikapo junuari 10 mwaka huu.
Katika hatua nyingine Mwamwaja alisema TTB imejipanga kuendelea kushirikiana na waandishi wa habari ili kuongeza idadi ya watalii lengo ni kuhakikisha wanatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020/2025 ya kufikia watalii milioni tano.
Alisema lengo lingine ni kuunga mkono jitihada za Rais Dk.Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha sekta ya utalii inakua na kuchangia katika Uchumi wa taifa.
“Tunaamini kupitia waandishi wa habari tunaweza kuwafikia wananchi wengi na kutangaza vivutio vya utalii ili kuunga mkono jitihada za Rais Dk.Samia za kutangaza vivutio vya utalii na kuongeza idadi ya watu wanaotembelea,”alisema
Aliongeza kuwa:”Tunatamani kuona wananchi wanachangamkia fursa ya kutembelea vivutio vya utalii,”alisema
WAGOMBEA NAFASI YA NGAZI YA URAIS CCM KUTAMBULISHWA KWENYE MIAKA 48 YA CHAMA HICHO.
SERIKALI KUFANYA SENSA YA UZALISHAJI VIWANDA KWA MWAKA WA REJEA 2023.
AZANIA BENKI BUNGE BONANZA LAWALETA PAMOJA MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA.
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUKUTANA KATIKA BONANZA LA KUHAMASISHA MICHEZO NA UMUHIMU WA MAZOEZI.
MABADILIKO YA SERA YA ELIMU KUAKISI MABADILIKO YA KITAIFA NA KIMATAIFA.
WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU
RASMI UZINDUZI WA SERA YA ELIMU KUFANYIKA TAREHE 1 FEBRUARI 2025.
WASIRA: CHADEMA MSIJE NA AZIMIO LINALOKIUKA SHERIA ZA NCHI YETU.