

Utendaji kazi wa kiwango cha juu wa Rais Samia Suluhu Hassan, umewezesha eneo kubwa la nchi kuwa na uhakika wa kupata maji safi na salama kwa mijini na vijijini hali iliyoifanya Serikali kutaka mafanikio hayo yalindwe.
Ikumbukwe kuwa hadi kufikia Februari 2024, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika maeneo ya vijijini ilifikia asilimia 79.6 ikilinganishwa na asilimia 77 Februari, 2023.
Kwa upande wa mijini upatikanaji wa maji umefikia asilimia 90 ikilinganishwa na asilimia 88 Februari 2023.
Mafanikio hayo ni makubwa na ndio yamempa nguvu Kaibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri kuwataka watumishi wa Sekta ya Maji kuhakikisha wanalinda mafanikio yaliyofikiwa katika utekelezaji wa majukumu ya sekta hiyo.
Mhandisi Mwajuma ametoa agizo hilo katika kikao chake na watumishi wa Wizara hiyo jijini Dodoma.
Ikumbukwe kuwa Serikali ya Rais Samia, kupitia Wizara ya Maji, imeweka malengo makubwa ya kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa uhakika wa maji safi na salama kwa wananchi wote nchini.
Malengo haya ni sehemu ya juhudi za kufikia Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025 na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).
Kwa mujibu wa mpango wa serikali ni kuhakikisha huduma ya maji safi na salama inawafikiwa asilimia 95% ya wakazi wa mijini ifikapo mwaka 2025.
Kwa upande wa wananchi wa Vijijini asilimia 85 wawe wanapata huduma ya maji safi na salama ifikapo mwaka 2025.
Malengo hayo yanategemewa kufanikishwa na miradi mbalimbali kama Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP), ambayo inalenga kuboresha miundombinu ya maji na kuongeza upatikanaji wa maji vijijini na mijini.
Serikali pia inashirikiana na sekta binafsi na mashirika ya kimataifa ili kufanikisha malengo haya.
#KAZIINAONGEA
NCAA IMEFANIKIWA Kudhibiti Ujangili wa Wanyamapori Ndani na Nje ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Vituo 94 vimepewa mikopo na NHIF kwa ajili ya kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi.
GHARAMA YA KUPANDIKIZA MIMBA NI MILIONI 14 MUHIMBILI.
UPOTEVU Wa Maji Kwa Mwaka 2021 Ulikuwa Wastani wa Asilimia 64.
MOI Imefanikiwa Kuanzisha Huduma Zaidi ya 10 lkiwemo Upasuaji wa Ubongo Bila Kufungua Fuvu.
UPOTEVU Wa Maji Kwa Mwaka 2021 Ulikuwa Wastani wa Asilimia 64.
MOI Imefanikiwa Kuanzisha Huduma Zaidi ya 10 lkiwemo Upasuaji wa Ubongo Bila Kufungua Fuvu.
GHARAMA YA KUPANDIKIZA MIMBA NI MILIONI 14 MUHIMBILI.
WANANCHI WAILILIA SERIKALI,WAFUKUZWA KWENYE MAENEO YAO.
MAKAMPUNI MENGI YA KIGENI YANAHITAJI MAFUNDI WENYE UJUZI UNAOKUBALIKA KIMATAIFA.