NIC YAZINDUA KAMPENI YA NIC KITAA ILI KUTOA ELIMU YA BIMA KWA WANANCHI. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Biashara

NIC YAZINDUA KAMPENI YA NIC KITAA ILI KUTOA ELIMU YA BIMA KWA WANANCHI.

SHIRIKA la BIMA la Taifa (NIC), limezindua msimu wa pili wa kampeni ya NIC Kitaa yenye lengo la kutoa elimu ya bima kwa wananchi wote kwa kuwafuata kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo mitaani na kwenye shughuli zao za kiuchumi.

Sophia Kingimali
By Sophia Kingimali
12 Nov 2024
NIC YAZINDUA KAMPENI YA NIC KITAA ILI KUTOA ELIMU YA BIMA KWA WANANCHI.

Hayo ameyabainisha leo Novemba, 12 2024 jijini Dar es Salaam na Mtendaji Mkuu wa NIC Kaimu Mkeyenge amesema wananchi wa Tanzania  wana uelewa wa asilimia mbili  kuhusu elimu ya bima hivyo wamejipanga kuhakikisha wanatoa elimu hiyo kwa wananchi wote ili kufikia asilimia tano.

Amesema  wameingia msimu  wa pili wa kampeni wa NIC Kitaa kusogeza  huduma kwa wananchi na kuhakikisha elimu  ya bima inawafikia wananchi wote ili watambue umuhimu wa bima.

"Uelewa wa bima bado uko chini sisi kama Taasisi kongwe ya serikali  tunawajibu wa kusaidia serikali kwa sababu  bima ni ukusanyaji wa fedha za wananchi ambao wanahisi wakipata majanga wasaidiwe na faida yake inaweza kusaidia uchumi ambao unawekezwa katika mabenki mbalimbali hivyo tunaongeza mtaji kwenye  soko hususan sekta ya  bima,"'amesema.

Aidha Mkeyenge amesema  kutoa elimu  hiyo ni kuendeleza sera ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan  ya kuhakikisha bima  kwa wote na kuhakikisha watanzania wote wanatumia bima.

Ameongeza kuwa pamoja na kutoa elimu ya kampeni  hiyo wataambatisha na kuandikisha bima kwa wateja wapya lakini pia wanapokea malalamiko na kuyapatia ufumbuzi hapohapo lakini pia kulipa madeni  sio lazima wafike  ofisini  kwani wamewasogezea huduma.

Ameeleza kuwa kampeni hiyo inatarajia kufanyika kufayika nchi nzima lakini kwa sasa wameanza na mikoa ya Dar es Salaam,  Morogoro, Dodoma na Singida.

GAVANA TUTUBA: RIBA YA BENKI KUU KUENDELEA KUWA ASILIMIA 6.

GAVANA TUTUBA: RIBA YA BENKI KUU KUENDELEA KUWA ASILIMIA 6.

SAYANSI YA BAHARI NGUZO YA UCHUMI WA BLUU-RAIS MWINYI

SAYANSI YA BAHARI NGUZO YA UCHUMI WA BLUU-RAIS MWINYI

Watumishi wa Umma Waaswa kujifunza mifumo mipya ya Tehama ili kuwafikia wananchi kwa ukaribu.

Watumishi wa Umma Waaswa kujifunza mifumo mipya ya Tehama ili kuwafikia wananchi kwa ukaribu.

BoT KUJA NA MFUMO WA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO YA KIFEDHA KIDIGITAL.

BoT KUJA NA MFUMO WA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO YA KIFEDHA KIDIGITAL.

UZINDUZI WA TEKNOLOJIA MPYA YA UREKEBISHAJI NA UTUNZAJI WA MAGARI  KULETA MAPINDUZI MAKUBWA KATIKA SEKTA YA HUDUMA ZA MAGARI.

UZINDUZI WA TEKNOLOJIA MPYA YA UREKEBISHAJI NA UTUNZAJI WA MAGARI KULETA MAPINDUZI MAKUBWA KATIKA SEKTA YA HUDUMA ZA MAGARI.