

Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema kuwa kwa kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, Sekta ya Uchukuzi nchini imechangia kiasi cha dola za Marekani bilioni 2.48 za fedha za kigeni. Kiasi hicho ni sawa na ongezeko la asilimia 8.3 ikilinganishwa na dola bilioni 2.29 zilizopatikana katika kipindi kama hicho cha mwaka wa fedha 2023/2024.
Hayo yamebainishwa wakati wa Hotuba ya Waziri huyo akiwasilisha Bungeni Mpango wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa mwaka wa fedha 2025/26.
Ameeleza kuwa Sekta ya Uchukuzi ina mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta nyingine, ikiwemo sekta ya utalii, ambapo mapato ya mauzo ya usafirishaji huainishwa kila mwaka kupitia taarifa ya pamoja inayotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Waziri huyo amebainisha kuwa mchango wa fedha za kigeni unaotokana na sekta ya uchukuzi unatokana na mapato ya kodi mbalimbali, ikiwemo ushuru wa forodha, kodi ya ongezeko la thamani (VAT), pamoja na kodi nyingine zinazotokana na bidhaa kama mafuta ya petroli na dizeli.
Aidha Bunge la Tanzania limepitisha Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi ya Sh. trilioni 2.746 kwaajili ya matumizi ya mwaka 2025/26.
Wakati wa hitimisho la Mjadala wa Bajeti hiyo, Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa, amewashukuru wabunge wote 15 waliochangia Mjadala wa Bajeti hiyo, akiahidi kuwa wizara yake itayafanyia kazi maoni, mapendekezo na ushauri uliotolewa, ikiwmo kupunguza kuchelewa kwa safari za ndege zenye kuendeshwa na Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) .
Awali wizara hiyo pia imebainisha kwamba kwa mwaka ujao wa fedha, pamoja na mambo mengine itaendeleza ujenzi wa Reli ya Kisasa SGR katika ushoroba wa kati, kununua vitendea kazi pamoja na kuboresha reli zilizopo, kuifanyia maboresho ATCL, kuboresha miundombinu na huduma za bandari pamoja na kuendeleza ujenzi wa meli mpya na maboresho ya viwanja vya ndege na Meli zilizopo.
Kwa upande wake Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson, ameipongeza wizara hiyo kwa wasilisho na majukumu ambayo wamekuwa wakiyatekeleza.
Aidha, amemtakia Waziri na Naibu Waziri wake kila lenye kheri katika kutimiza yale yaliyomo kwenye mipango ya wizara kwa mwaka ujao wa fedha.
Rais Samia Asisitiza Mchujo wa Wagombea Kufanyika Kwa Haki.
Ilani Ya CCM Imeandaliwa Kwa Weledi Mkubwa Kwa Kushirikiana Na Wananchi;RAIS Dkt.Samia
WIZARA YA ARDHI YAJA NA VIPAUMBELE SABA
SERIKALI NA WADAU WAENDELEZA MAPAMBANO YA KIJINSIA
KAPINGA ATAJA VIGEZO VYA ZIADA UPELEKAJI UMEME VITONGOJINI.
WALIOHITIMU KIDATO CHA SITA WAITWA JKT
WIZARA YA ARDHI YAJA NA VIPAUMBELE SABA
Ilani Ya CCM Imeandaliwa Kwa Weledi Mkubwa Kwa Kushirikiana Na Wananchi;RAIS Dkt.Samia
SERIKALI NA WADAU WAENDELEZA MAPAMBANO YA KIJINSIA
Rais Samia Asisitiza Mchujo wa Wagombea Kufanyika Kwa Haki.