(LHRC) chatoa maelekezo kwa vyombo vya ulinzi na usalama Kufuatia mauaji ya watoto watatu wa familia moja | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

(LHRC) chatoa maelekezo kwa vyombo vya ulinzi na usalama Kufuatia mauaji ya watoto watatu wa familia moja

Kufuatia mauaji ya watoto watatu wa familia moja yaliyotokea usiku wa kuamkia jumatatu ya Septemba 16, 2024 Kata ya Nala Jijini Dodoma, Kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) kimelaani tukio hilo na kutaka vyombo vya ulinzi na usalama kubaini chanzo cha mauaji hayo.

The Dododma Post
By The Dododma Post
17 Sep 2024
(LHRC) chatoa maelekezo kwa vyombo vya ulinzi na usalama Kufuatia mauaji ya watoto watatu wa familia moja

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho, Dk Anna Henga leo jumanne Septemba 17, 2024 taarifa hiyo imesema hivi karibuni kumekuwepo ongezeko kubwa la matukio ya kikatili nchini hususani ya mauaji, watu kupotea na kutekwa.

Taarifa hiyo imesema matukio hayo yanaongeza hofu kubwa kwa wananchi kwani yanatishia usalama wao na jamii nzima na kwamba ongezeko la matukio hayo pia kwa sehemu yanaashiria udhaifu wa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ambavyo jukumu lao kubwa ni kuhakikisha kunakuwepo na ulinzi thabiti wa rai ana mali zao.

Kituo hicho kimetoa rai kwa mamlaka za ulinzi na usalama kuchunguza kwa kina tukio hilo ili kubaini chanzo cha mauaji hayo na kuhakikisha wahusika wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kwa mujibu wa sheria za nchi.

Pia wamevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuimarisha ulinzi wa raia kwa kuchukua hatua za haraka na Madhubuti pindi matukio yanapotolewa taarifa ili kupunguza hali ya wananchi kuchukua sheria mkononi mwao na kuhakikisha raia wanalindwa na wanaishi kwa amani na usalama.

“Jamii nzima kuheshimu sheria na kuepuka kujichukulia sheria mkononi... badala ya kulipa visasi na kufanya matukio ya kikatili watafute suluhu za kisheria katika kutatua migogoro pia kutoa taarifa kwa vyombo husika kuhusu matukio kama haya maana kujichukulia sheria mkononi ni kuzidisha matatizo na kuhatarisha amani katika jamii,” imesema taarifa hiyo.

Aidha viongozi wa dini na wa kijamii kuendelea kuhubiri amani na kuhamasisha umuhimu wa amani kutii sheria na kuzuia vitendo vya ukatili na kujichukulia sheria mkononi kwani vinakwenda kinyume na maadili ya jamii zetu, misingi ya Imani za dini n ani kinyumecha sheria.

“Kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC)kinasisitiza umuhimu wa kuendeleza utulivu, haki na usalama wa raia kwa kushirikiana na vyombo vya dol ana kuheshimu misingi ya haki za binadamu,” imesema taarifa hiyo

FURAHIKA WAJIVUNIA MAFANIKIO ASILIMIA 75 YA WAHITIMU WAKE KAPATA AJIRA.

FURAHIKA WAJIVUNIA MAFANIKIO ASILIMIA 75 YA WAHITIMU WAKE KAPATA AJIRA.

EKARI 1,165 za mashamba ya bangi zateketezwa Morogoro

EKARI 1,165 za mashamba ya bangi zateketezwa Morogoro

DCEA YAFANYA OPARESHENI MAALUM YA SIKU TISA MKOANI MOROGORO.

DCEA YAFANYA OPARESHENI MAALUM YA SIKU TISA MKOANI MOROGORO.

FCS KUADHIMISHA WIKI YA AZAKI SEPTEMBA 9,ARUSHA.

FCS KUADHIMISHA WIKI YA AZAKI SEPTEMBA 9,ARUSHA.

JAMII YA KIMASAI IMEANZA KUENDANA NA KASI YA UTANDAWAZI.

JAMII YA KIMASAI IMEANZA KUENDANA NA KASI YA UTANDAWAZI.