MTAALA MPYA WA ELIMU WAANZA KUTUMIKA (MUHAS) | The Dodoma Post
The Dodoma Post Makala

MTAALA MPYA WA ELIMU WAANZA KUTUMIKA (MUHAS)

Sera mpya ya Elimu na Mafunzo nchini, imeshaanza kutekelezwa nchini, kutokana na kufanyiwa kwa marekebisho kwa sera ya mwaka 2014 toleo la mwaka 2023.

Gilbert ludovick
By Gilbert ludovick
27 Aug 2024
MTAALA MPYA WA ELIMU WAANZA KUTUMIKA (MUHAS)

Sera hiyo ilivyotoka ilisababisha mtaala kubadilishwa kuanzia ngazi za chini hadi vyuo na hivi sasa Taasisi za elimu ya juu nazo kuendana na Sera za elimu nchini.

Laurence Msofe ambaye ni Mkurugenzi wa elimu ya juu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia amesema hayo wakati alipokuwa mgeni Rasmi kwenye kongamano la mradi wa mabadiliko katika ufundishaji wa wataalamu wa Afya.

Msofe amebainisha kuwa, mradi huo umeendeshwa kwa miaka 6 na unahusisha Chuo Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), lakini pia Chuo cha KUHAS, KCMS pamoja na vyuo viwili kutoka nje ya nchi ikiwa ni pamoja na Chuo cha DUKES na Chuo cha St. Francisco University of California Marekani.

"Maengo ya huu mradi ni kufanya mapitio makubwa katika namna ya kufundisha wataalamu wa Afya na kwajili ya kupata wataalamu wa Afya ambao wana ujuzi lakini pia wana uwezo wa kutenda kazi zao kwa umahiri mkubwa," ameeleza Msofe na kuongeza,

"Mradi huu umefanikiwa kutengeneza mitaala ya mfano katika mafunzo ya udaktari, lakini pia mafunzo ya uuguzi na ni mitaala ambayo imeshapitishwa na Taasisi yetu ya tume ya vyuo vikuu Tanzania na tunatarajia kwamba itatumika sasa sio tu kwa vyuo hivyo ambavyo nimevitaja lakini pia kwa vyuo vingine hapa Tanzania."

Katika Mradi huo ambao umefadhiliwa umelenga kuangalia ameongeza namna ya kupata tofauti ya ufundishaji katika masomo hayo ya tiba hasa kwa udaktari na uuguzi.

Naye Prof. Gideon Kwesigabo mratibu wa mradi huo amesema katika utekelezaji wake wamefuata njia tatu ambazo ni kubadilisha mtaala, kuongeza uwezo wa walimu kufundisha pamoja na kuhusisha wadau kuhakikisha kwamba wanashiriki katika mradi huo.

Aidha amesema kuwa kwa sasa wanashirikiana na wahitimu mbalimbali kutoka katika vyuo ili waweze kusaidia katika kuboresha mfumo wa elimu katika ngazi ya vyuo nchini.

Kwa upande wake Prof. Appolinary Kamuhabwa Makamu Mkuu MUHAS amesema malengo ya mradi ni kuangalia namna bora ya ufundishaji unaofanyika lakini pia namna wanavyowataini wataalamu wa afya na vitu gani wanatakiwa kuvijua kulingana na mazingira ya   Tanzania na ulimwenguni, hivyo mradi umewasaidia kuweza kutekeleza mitaala pamoja na wataalamu wa kufundisha.

"Huu mradi tunaona kwa kiasi kikubwa unaenda kuinua ubora wa mafunzo ya afya kwa elimu ya juu hapa nchini na tunaishukuru Wizara ya elimu kwa kulipokea vizuri na baada ya kongamano hili tutawasilisha mapendekezo" Amesisitiza

Dkt. Ndumbaro: Nitatembelea Mradi Huu Kila Baada ya Wiki Mbili

Dkt. Ndumbaro: Nitatembelea Mradi Huu Kila Baada ya Wiki Mbili

Safari ya Omary Katanga Barani Afrika na Maandalizi ya Afcon 2027-2

Safari ya Omary Katanga Barani Afrika na Maandalizi ya Afcon 2027-2

Safari ya Omary Katanga Barani Afrika na Maandalizi ya Afcon 2027

Safari ya Omary Katanga Barani Afrika na Maandalizi ya Afcon 2027

Afcon 2027 Kuchele, Kamati ya Afcon 2027 Yakabidhiwa Maandalizi

Afcon 2027 Kuchele, Kamati ya Afcon 2027 Yakabidhiwa Maandalizi

Zipi 	Faida na Fursa za Afcon 2027 Tanzania?

Zipi Faida na Fursa za Afcon 2027 Tanzania?