BASHUNGWA KUSIMAMIA MAELEKEZO YA DKT. NCHIMBI, BARABARA INAYOUNGANISHA KAGERA - KIGOMA KUKAMILIKA OKTOBA, 2024 | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

BASHUNGWA KUSIMAMIA MAELEKEZO YA DKT. NCHIMBI, BARABARA INAYOUNGANISHA KAGERA - KIGOMA KUKAMILIKA OKTOBA, 2024

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemuhakikishia Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi itahakikisha inasimamia kikamilifu ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami inayounganisha Mkoa wa Kagera na Kigoma kupitia Kibondo kukamilika ifikapo mwezi Oktoba, 2024.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
09 Aug 2024
BASHUNGWA KUSIMAMIA MAELEKEZO YA DKT. NCHIMBI, BARABARA INAYOUNGANISHA KAGERA - KIGOMA KUKAMILIKA OKTOBA, 2024

Bashungwa amezungumza hayo Agosti 09, 2024 Wilayani Misenyi Mkoani Kagera wakati akitoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Nchimbi kufuatia maelekezo aliyoyatoa Mkoani Kigoma kwa Wizara ya Ujenzi.

“Mheshimiwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi tunakuhakikishia maelekezo uliyoyatoa Mkoani Kigoma ya kukamilisha barabara inayounganisha Mkoa wa Kagera na Kigoma, tunakuahidi ikifika mwezi wa kumi barabara ya kutoka Kagera hadi kibondo itakuwa imeshakamilika”, amesema Bashungwa.

Bashungwa ameahidi kushughulikia fidia kwa wananchi waliopisha ujenzi wa barabara ya Mabamba - Kibondo pamoja na malipo ya Mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa barabara ya Kibondo Townlink Mkoani Kigoma.

Kuhusu Mkoa wa Kagera, Waziri Bashungwa ameeleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuunganisha Wilaya ya Misenyi na Bukoba vijijini kwa barabara ya kiwango cha lami kuanzia Kyaka - Katoro hadi Kyetema (km 60.7) ambapo katika Bajeti ya Serikali ya mwaka 2024-2025 itaanza ujenzi wa barabara hiyo kipande cha kilometa 10 pamoja na ujenzi wa Daraja la Kalebe.

Aidha, Bashungwa amesema Serikali inaendelea na utekelezaji wa miundombinu ya barabara na madaraja ikiwa ni pamoja na upanuzi wa barabara njia nne kuanzia Rwamishenye Roundabout hadi Stendi Mpya ya Bukoba Mjini, barabara ya Karagwe - Benaco (km 60) pamoja na ukarabati wa barabara ya Lusahunga - Rusumo (km 92).

Bashungwa ameeleza kuwa Serikal inafungua barabara ya Nyabihanga - Minziro kwa kuanza na kilometa sita kuanzia Mtukula mpaka Minziro na hivi sasa Wakandarasi wapo katika barabara hiyo kuendelea kurekebisha maeneo yote korofi.

Kuhusu ufungaji wa taa za barabarani katika maeneo ya Kyaka, Bunazi na Mtukula, Bashungwa ameeleza kuwa TANROADS wanakamilisha hatua za manunuzi kwa ajili ya kufunga taa hizo ikiwa ni ombi la Mbunge wa Jimbo la Nkenge Wilayani Misenyi, Dkt. Florent Kyombo.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Nkenge Wilayani Misenyi Dkt. Florent Kyombo ametoa ombi la Mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa barabara ya Bunazi - Kagera Sugar hadi njia panda ya Kitengule kwa kiwango cha lami kulipwa malipo ya awali ili ujenzi wa barabara hiyo uweze kuanza.

JESHI LA POLISI LATOA TAMKO UTATA WA KIFO CHA MSANII MANDOJO.

JESHI LA POLISI LATOA TAMKO UTATA WA KIFO CHA MSANII MANDOJO.

RC CHALAMILA AIPONGEZA TPDC KWA KUTOA ELIMU YA UTUNZAJI MIUNDOMBINU YA SHIRIKA HILO.

RC CHALAMILA AIPONGEZA TPDC KWA KUTOA ELIMU YA UTUNZAJI MIUNDOMBINU YA SHIRIKA HILO.

Asali ya Tanzania Yapata Kibali Kuuzwa China.

Asali ya Tanzania Yapata Kibali Kuuzwa China.

BENKI YA BIASHARA TANZANIA (TCB) KUSHIRIKIANA NA  BUNGE LA TANZANIA KUWAINUA WAJASIRIAMALI NCHINI.

BENKI YA BIASHARA TANZANIA (TCB) KUSHIRIKIANA NA BUNGE LA TANZANIA KUWAINUA WAJASIRIAMALI NCHINI.

REA YAAHIDI KUENDELEA KUWAWEZESHA WAENDELEZAJI BINAFSI WA UMEME NCHINI.

REA YAAHIDI KUENDELEA KUWAWEZESHA WAENDELEZAJI BINAFSI WA UMEME NCHINI.