RC SENYAMULE ATAMANI DODOMA KUWA JIJI LA KIBIASHARA. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Biashara

RC SENYAMULE ATAMANI DODOMA KUWA JIJI LA KIBIASHARA.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wafanyabiashara na taasisi za fedha kutumia fursa za miundombinu na uwepo wa makao makuu ya serikali Jijini hapo kuwekeza kwenye miradi itakayo wezesha Jiji hilo kuwa la kibiashara.

Na Moreen Rojas, Dodoma.
By Na Moreen Rojas, Dodoma.
26 May 2024
RC SENYAMULE ATAMANI DODOMA KUWA JIJI LA KIBIASHARA.

Wito huo umetolewa leo tarehe 25.05.2024 wakati wa maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa chama cha ushirika, akiba na mikopo (SACCOS) ya kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Arusha Road Jijini Dodoma .

Mhe.Senyamule amesema Jiji la hilo lina fursa mbalimbali za miundombinu ikiwemo ya barabara,reli na viwanja vya ndege ambayo ikitumika vyema na wafanyabiashara na taasisi hizo itasaidia kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

"Hadi kufikia mwakani kiwanja cha ndege msalato kitakuwa kimekamilika, hivyo tunapaswa kutumia fursa hiyo kwa kujenga hoteli za kisasa na kuangalia namna ambayo Dodoma inaweza kuwa tofauti haswa kwenye uwekezaji na biashara, tunataka Dodoma iwe kitovu cha kila kitu na haya yote yanawezekana chini ya Saccos kubwa kama KKKT Arusha Road Saccos" Ameeleza  Senyamule

Ametoa shime kwa wanachama wa SACCOS hiyo kuendelea kuweka akiba pamoja na kukopa na kurejesha kwa wakati mikopo hiyo Ili kupata faida itakayowawezesha kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na kijamii ikiwamo ya kurejesha uisani kwa Jamii (CSR)

Kwa upande wake Mwakilishi wa mtendaji Mkuu wa tume ya maendeleo ya ushirika (TCDC) Bw. Kisamalala Josephat amewapongeza viongozi wa Saccos hiyo kwa kufuata sheria za Ushirika ikiwemo kuwahamasisha wanachama kushirikiana na kurejesha mkopo kwa wakati.

Naye Afisa ushirika Mkuu Halmashauri  jiji la Dodoma Bw.Joseph Chitinka  awewashauri kutafuta watalaam watakaowasaidia kubuni miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ujenzi wa hoteli l, uwekezaji wa kibiashara Ili kujijenga kiuchumi.

Maadhimisho hayo yenye kaulimbiu "BORESHA MAISHA NA KKKT ARUSHA ROAD SACCOS LTD" ilitanguliwa  na semina kwa wana Chama hao.

SERIKALI KUENDELEA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI MTWARA.

SERIKALI KUENDELEA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI MTWARA.

PPRA kuandaa na kuratibu jukwaa la ununuzi wa Umma la afrika mashariki.

PPRA kuandaa na kuratibu jukwaa la ununuzi wa Umma la afrika mashariki.

FCC YAWATAKA WADAU KUSHIRIKIANA KUTOKOMEZA BIDHAA BANDIA.

FCC YAWATAKA WADAU KUSHIRIKIANA KUTOKOMEZA BIDHAA BANDIA.

TRA YAENDELEA NA UTEKELEZAJI WA MAAGIZO YA SERIKALI KUHUSU WAFANYABIASHARA.

TRA YAENDELEA NA UTEKELEZAJI WA MAAGIZO YA SERIKALI KUHUSU WAFANYABIASHARA.