

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wafanyabiashara na taasisi za fedha kutumia fursa za miundombinu na uwepo wa makao makuu ya serikali Jijini hapo kuwekeza kwenye miradi itakayo wezesha Jiji hilo kuwa la kibiashara.
Wito huo umetolewa leo tarehe 25.05.2024 wakati wa maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa chama cha ushirika, akiba na mikopo (SACCOS) ya kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Arusha Road Jijini Dodoma .
Mhe.Senyamule amesema Jiji la hilo lina fursa mbalimbali za miundombinu ikiwemo ya barabara,reli na viwanja vya ndege ambayo ikitumika vyema na wafanyabiashara na taasisi hizo itasaidia kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
"Hadi kufikia mwakani kiwanja cha ndege msalato kitakuwa kimekamilika, hivyo tunapaswa kutumia fursa hiyo kwa kujenga hoteli za kisasa na kuangalia namna ambayo Dodoma inaweza kuwa tofauti haswa kwenye uwekezaji na biashara, tunataka Dodoma iwe kitovu cha kila kitu na haya yote yanawezekana chini ya Saccos kubwa kama KKKT Arusha Road Saccos" Ameeleza Senyamule
Ametoa shime kwa wanachama wa SACCOS hiyo kuendelea kuweka akiba pamoja na kukopa na kurejesha kwa wakati mikopo hiyo Ili kupata faida itakayowawezesha kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na kijamii ikiwamo ya kurejesha uisani kwa Jamii (CSR)
Kwa upande wake Mwakilishi wa mtendaji Mkuu wa tume ya maendeleo ya ushirika (TCDC) Bw. Kisamalala Josephat amewapongeza viongozi wa Saccos hiyo kwa kufuata sheria za Ushirika ikiwemo kuwahamasisha wanachama kushirikiana na kurejesha mkopo kwa wakati.
Naye Afisa ushirika Mkuu Halmashauri jiji la Dodoma Bw.Joseph Chitinka awewashauri kutafuta watalaam watakaowasaidia kubuni miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwamo ujenzi wa hoteli l, uwekezaji wa kibiashara Ili kujijenga kiuchumi.
Maadhimisho hayo yenye kaulimbiu "BORESHA MAISHA NA KKKT ARUSHA ROAD SACCOS LTD" ilitanguliwa na semina kwa wana Chama hao.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege