BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AKAGUA ENEO LILILOATHIRIKA NA MAJI WILAYA YA KIGAMBONI JIJINI DAR ES SALAAM. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AKAGUA ENEO LILILOATHIRIKA NA MAJI WILAYA YA KIGAMBONI JIJINI DAR ES SALAAM.

Mkurugenzi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Brigedia Jenerali Hosea Ndagala tarehe 9 Mei, 2024 amefanya ziara ya kutembelea Wilaya ya Kigamboni kata ya Mjimwema Mtaa wa Maweni kwa lengo la kuangalia madhara yaliyotokea kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha Jijini Dar es Salaam.

The Dododma Post
By The Dododma Post
10 May 2024
BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AKAGUA ENEO LILILOATHIRIKA NA MAJI WILAYA YA KIGAMBONI JIJINI DAR ES SALAAM.

Awali akiwa katika kikao cha pamoja na Katibu Tawala Msaidizi (Mipango na Uratibu) Ndg. Chillah Moses katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwaajili ya kupata taarifa kuhusu hali halisi ya madhara ya mvua hizo kwa Wilaya ya Kigamboni alielezwa kuwa maeneo yaliyoathiriwa ni pamoja na Mtaa wa Maweni eneo la Bondeni  kata ya Mji Mwema pamoja na Maweni eneo la Biasi  ambayo yamezingirwa na maji  ya mvua zinazoendelea kunyesha Katika Mkoa huo.

Mkurugenzi Idara ya Menejimenti ya Maafa  Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu ) Brigedia Jenerali Hosea (wa kwanza kushoto) pamoja na waratibu wa Maafa Mkoa wa Dar es Salaam Ndg. Gerlad Sondo (mwenye suti) wakikagua maeneo hayo yaliozingirwa na Maji katika eneo la Mtaa wa Maweni Bondeni.

Aidha Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu itaendelea kuratibu masuala ya menejimenti ya maafa nchini ili kuhakikisha jamii inaendelea kuwa salama na stahimilivu dhidi ya maafa.

Baadhi ya Nyumba zilizozingirwa na Maji katika eneo la Mtaa wa Maweni Bondeni kata ya Mji Mwema Wilaya ya
Kigambini mkoa wa Dar es Salaam.
DKT.TULIA AMUAPISHA BALOZI KOMBO AMTAKA KUCHAPA KAZI.

DKT.TULIA AMUAPISHA BALOZI KOMBO AMTAKA KUCHAPA KAZI.

RAIS DK.SAMIA awaongoza watanzania maadhimisho ya siku ya mashujaa.

RAIS DK.SAMIA awaongoza watanzania maadhimisho ya siku ya mashujaa.

HISTORIA IMEANDIKWA SGR YAZINDUA SAFARI ZAKE RASMI DAR ES SALAAM-DODOMA.

HISTORIA IMEANDIKWA SGR YAZINDUA SAFARI ZAKE RASMI DAR ES SALAAM-DODOMA.

RAIS DKT SAMIA ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA

RAIS DKT SAMIA ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA

DIWANI MAKURUMLA AWATOA HOFU WAZAZI UTEKAJI WA WATOTO.

DIWANI MAKURUMLA AWATOA HOFU WAZAZI UTEKAJI WA WATOTO.