![The Dododma Post](https://thedodomapost.co.tz/media/prof/logo.png)
![BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AKAGUA ENEO LILILOATHIRIKA NA MAJI WILAYA YA KIGAMBONI JIJINI DAR ES SALAAM.](https://thedodomapost.co.tz/media/news/1715360923.jpg)
Mkurugenzi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Brigedia Jenerali Hosea Ndagala tarehe 9 Mei, 2024 amefanya ziara ya kutembelea Wilaya ya Kigamboni kata ya Mjimwema Mtaa wa Maweni kwa lengo la kuangalia madhara yaliyotokea kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha Jijini Dar es Salaam.
Awali akiwa katika kikao cha pamoja na Katibu Tawala Msaidizi (Mipango na Uratibu) Ndg. Chillah Moses katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwaajili ya kupata taarifa kuhusu hali halisi ya madhara ya mvua hizo kwa Wilaya ya Kigamboni alielezwa kuwa maeneo yaliyoathiriwa ni pamoja na Mtaa wa Maweni eneo la Bondeni kata ya Mji Mwema pamoja na Maweni eneo la Biasi ambayo yamezingirwa na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha Katika Mkoa huo.
Aidha Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu itaendelea kuratibu masuala ya menejimenti ya maafa nchini ili kuhakikisha jamii inaendelea kuwa salama na stahimilivu dhidi ya maafa.
MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEKUA DED MAFIA KASSIM NDUMBO
RAIS DKT SAMIA ATAJWA SHUJAA WA UWEKEZAJI.
DKT.TULIA AMUAPISHA BALOZI KOMBO AMTAKA KUCHAPA KAZI.
RAIS DK.SAMIA awaongoza watanzania maadhimisho ya siku ya mashujaa.
KAGERA, GEITA WATAKIWA KUTUNZA VIFAA VYA UBORESHAJI
DIRA YA TAIFA 2050 NI MAONO YA NCHI SIKU ZA USONI - DKT. BITEKO
WAZIRI BASHE ATANGAZA NEEMA KILIMO CHA UMWAGILIAJI KATAVI.
HISTORIA IMEANDIKWA SGR YAZINDUA SAFARI ZAKE RASMI DAR ES SALAAM-DODOMA.
Vijiji 151 vimebaki nchi nzima kupata huduma ya umeme - Kapinga
WAZIRI MKUU AZINDUA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KIGOMA.