SERIKALI yainisha Mpango wa kuwasaidia wachimbaji wadogo wa Madini Nchini | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

SERIKALI yainisha Mpango wa kuwasaidia wachimbaji wadogo wa Madini Nchini

Waziri wa Madini Mhe.Anthony Mavunde ameainisha mpango wa Serikali wa kusaidia utatuzi wa changamoto zinazowakabili wachimbaji wadogo nchini.

The Dododma Post
By The Dododma Post
09 May 2024
SERIKALI yainisha Mpango wa kuwasaidia wachimbaji wadogo wa Madini Nchini

Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Mei 9, 2024 wakati akijibu swali la Dkt. Christine  Ishengoma Mbunge wa Viti Maalum aliyetaka kujua mpango wa Serikali kuwasaidia Wachimbaji Wadogo wa Madini Wilaya ya Ulanga.

Ameongeza kwamba, mpango wa Serikali ni kuwasaidia wachimbaji wadogo nchini wakiwemo wachimbaji wa madini wa Wilaya ya Ulanga unahusisha masuala mbalimbali ikiwemo 
Kuwekeza zaidi katika utafiti wa kina kugundua uwepo wa madini katika maeneo mbalimbali ili kuwaongoza vizuri wachimbaji wadogo.

“ Mhe. Spika maeneo mengine ni utoaji wa leseni za uchimbaji kwa wachimbaji wadogo; kutoa elimu ya matumzi ya teknolojia sahihi ya uchimbaji ili kuongeza tija; huduma ya uchorongaji kwa gharama nafuu kupitia Shirika la Madini la Taifa (STAMICO),” amesema Waziri Mavunde.

Vilevile, amesema kuwa, mpango mwingine ni kuwezesha upatikanaji wa mikopo nafuu kwa wachimbaji; na fursa ya ukodishaji wa mitambo na vifaa chini ya usimamizi wa STAMICO.

KAGERA, GEITA WATAKIWA KUTUNZA VIFAA VYA UBORESHAJI

KAGERA, GEITA WATAKIWA KUTUNZA VIFAA VYA UBORESHAJI

WANAOJIANDIKISHA KUWA WAPIGA KURA ZAIDI YA MARA MOJA KUTUMIKIA KIFUNGO JELA.

WANAOJIANDIKISHA KUWA WAPIGA KURA ZAIDI YA MARA MOJA KUTUMIKIA KIFUNGO JELA.

KAGERA, GEITA KUANZA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AGOSTI 5,2024

KAGERA, GEITA KUANZA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AGOSTI 5,2024

KADI ZA MPIGA KURA ZENYE JINA LA ZAMANI LA TUME NI HALALI

KADI ZA MPIGA KURA ZENYE JINA LA ZAMANI LA TUME NI HALALI

KAILIMA: WENGI WAJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

KAILIMA: WENGI WAJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.