TUNAAMINI UCHAGUZI UTAKUWA WA AMANI NA USALAMA UTAKUWEPO- WANANCHI WA KIBAHA | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

TUNAAMINI UCHAGUZI UTAKUWA WA AMANI NA USALAMA UTAKUWEPO- WANANCHI WA KIBAHA

Wananchi wa Kibaha Mkoani Pwani wamesema wana uhakika kuwa uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utakuwa wa amani na haki kwa kila mmoja anayeshiriki uchaguzi huo, wakiamini kuwa siku ya Oktoba 29, 2025 kutakuwa na amani na utulivu pia kutokana na uthibitisho na uhakika walioupata kwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyesema kuwa serikali na Vyombo vya Dola vimejipanga kikamilifu kuhakikisha kila mwananchi anapata fursa ya kupiga kura katika mazingira salama na tulivu kote nchini.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
15 Oct 2025
TUNAAMINI UCHAGUZI UTAKUWA WA AMANI NA USALAMA UTAKUWEPO- WANANCHI WA KIBAHA

Wananchi wa Kibaha Mkoani Pwani wamesema wana uhakika kuwa uchaguzi Mkuu wa mwaka huu utakuwa wa amani na haki kwa kila mmoja anayeshiriki uchaguzi huo, wakiamini kuwa siku ya Oktoba 29, 2025 kutakuwa na amani na utulivu pia kutokana na uthibitisho na uhakika walioupata kwa Rais Samia Suluhu Hassan aliyesema kuwa serikali na Vyombo vya Dola vimejipanga kikamilifu kuhakikisha kila mwananchi anapata fursa ya kupiga kura katika mazingira salama na tulivu kote nchini.

Wananchi hao akiwemo Bi. Mwinyimvua Kasosoma na Mwanaidi Stephano, wakazi wa Kwa Mathias, Kibaha Mkoani Pwani wamesema hayo leo Oktoba 15, 2025 wakati wakizungumza na mwandishi wetu na kusisitiza kuwa wao na familia zao watajitokeza wote wenye sifa kwenda kupiga kura na kumchagua Kiongozi wanayeamini atawaletea maendeleo.

Aidha wamekumbusha umuhimu wa kuheshimu sheria na Miongozo yote ya Uchaguzi Mkuu, wakisema mara baada ya Kupiga kura ni muhimu kila mmoja kuondoka kwenye Vituo vya kupigia kura na kwenda kuendelea na shughuli nyingine za kiuchumi, wakijitenga na baadhi ya maneno ya wanasiasa wanaowataka wafuasi wao kusalia vituoni ili kuhakikisha ulinzi wa kura ama kuachana na upigaji wa kura na kuandamana ili kuitika hamasa ya baadhi ya wanaharakati na wanasiasa.

Uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa kuwachagua Madiwani, Wabunge na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unafanyika Oktoba 29, 2025 ambapo Rais wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya ulinzi na usalama Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari amewahakikishia wananchi wote usalama na utulivu wa kutosha siku hiyo, akionya wale wote wanaopanga kufanya vitendo vya uhalifu ama uvunjifu wa amani nchini.

Polisi Watuliza Hofu: Usalama Waimarishwa Kwa Uchaguzi Oktoba 29

Polisi Watuliza Hofu: Usalama Waimarishwa Kwa Uchaguzi Oktoba 29

Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha

Huduma za Uwakala CRDB Zachochea Ukuaji wa Mapato ya Serikali na Ujumuishi wa Kifedha

HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA

HAKUNA LITAKALOTOKEA OKTOBA 29, NENDENI MKAPIGE KURA- MSIGWA

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO

TUKACHAGUE VIONGOZI TUWATAKAO KUEPUSHA LAWAMA NA MALALAMIKO

Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya  VSOMO ya VETA

Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya VSOMO ya VETA