

Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini imetoa rai kwa wananchi kujitokeza kwenye maonesho ya 49 ya biashara sabasaba ili kupata elimu ya sheria zinazosimamiwa na ofisi hiyo hasa katika kipindi hiki tunapoelekea uchaguzi mkuu 2025.
Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini imetoa rai kwa wananchi kujitokeza kwenye maonesho ya 49 ya biashara sabasaba ili kupata elimu ya sheria zinazosimamiwa na ofisi hiyo hasa katika kipindi hiki tunapoelekea uchaguzi mkuu 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari leo julai 3,2025 Afisa Sheria Dinna Mcharo amesema ofisi hiyo inasimamia sheria mbalimbali za vyama vya siasa ikiwemo sheria ya vyama vya siasa sura ya 258 lakini pia sheria ya gharama za uchaguzi sura ya 278.
Amesema wameshiriki katika maonesho hayo ili kuendelea kutoa elimu kwa umma ili wapate kujua sheria zinazosimamiwa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi kuu.
"Mimi nitoe rai kwa wananchi wanaokuja kutembelea maonesho haya kuhakikisha wanapita hapa ili waje wapate elimu wajue sheria ziazowasimamia wanasiasa kipindi wanapotekeleza majukumu yao ya kisiasa hasa tunapoelekea uchaguzi mkuu",Amesema.
Aidha ameongeza kuwa ofisi ya msajili wa vyama inamajukumu mengi ikiwemo kusajili na kufuatilia utendaji wa vyama vya siasa kwa mujibu wa sheria lakini piakuratibu shughuli za baraza la vyama vya siasa.
Aidha ameongeza kuwa wanajukumu la kufuatilia mapato na matumizi ya vyama vya siasa lakini kugawa na kufuatilia matumizi ya fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa vyenye sifa.
CCM Yatangaza Wagombea Nafasi Ya Ubunge Waliopenya Kwenye Mchujo:Mpina,Makamba Waenguliwa.
KATIBU BAWACHA AJIUNGA CHAUMA ATAJA SABABU YA KUONDOKA KWAKE.
MASLAHI MAPANA YA NCHI YANAZINGATIWA UTEKELEZAJI WA MRADI WA EACOP-DKT. MATARAGIO.
VYAMA VYA SIASA VYAHAKIKISHIWA UWANJA SAWA UCHAGUZI MKUU 2025
INEC YATANGAZA RASMI TAREHE YA UCHAGUZI MKUU 2025.
CCM Yatangaza Wagombea Nafasi Ya Ubunge Waliopenya Kwenye Mchujo:Mpina,Makamba Waenguliwa.
SHUJAA ALIYEPIGANA VITA ASISITIZA AMANI.
VITUO VIWILI VYA KUPUNGUZA KASI YA MAFUTA GHAFI EACOP KUJENGWA NCHINI.
TBC KUAZIMISHA MIAKA 26 YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA HAYATI MWALIMU NYERERE KWA KUENDESHA MASHINDANO YA INSHA KWA WANAFUNZI.
SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WANANCHI YAINGIZA SEKTA BINAFSI KUENDESHA MRADI WA MWENDOKASI.