

WAZIRI wa Katiba na Sheria,Dk Damas Ndumbaro amesema kupitia kampeni ya Mama Samia Legal Aids Compain (MSLAC) wamebaini wananchi bado wanachangamoto za kisheria katika mambo manne ambayo ni ukatili wa kijinsia,migogoro ya ardhi, ndoa na ardhi.
Kauli hiyo ameitoa leo Jumatatu,Januari 20,2025 wakati akizungumza na Waandishi kuhusiana na kampeni ya Mama Samia Legal Aids Compain (MSLAC) katika mikoa 6 ambayo inatarajiwa kuanza Januari 24 mwaka huu.
Waziri Ndumbaro amesema kupitia kampeni hiyo walifika katika mikoa 11 na changamoto zilizojitokeza kwa wingi ni ukatili wa kijinsia,migogoro ya ardhi, ndoa na ardhi.
Amesema kwenye sekta ya ardhi wamebaini ubabaishaji ni mwingi ambapo amemwomba Waziri wa Ardhi,Deogratius Ndejembi kumtumia orodha ya migogoro sugu ili baada ya kampeni hiyo waanze kuishughulikia.
"Katika sera yetu ya utoaji haki tutahakikisha wananchi wanapata haki na wanapata elimu ya kisheria,"amesema Waziri Ndumbaro.
Amesema waliopo vijijini wana kiu ya haki ndio maana Rais aliunda Tume ya Haki jinai ambayo ilibainisha umuhimu wa haki kumfikia Mwananchi.
Amesema kupitia kampeni hiyo waliweza kuwafikia watu 175,119 ambapo asilimia 49 ni wanawake na 51 ni wanaume ambapo walitatua jumla ya migogoro 3162
Dkt. Ndumbaro amesema mpaka sasa Kampeni hiyo imeshawafikia Watanzania takribani 775,119 wakiwemo Wanawake 380,375 na Wanaume 394,744 ambapo jumla ya Migogoro 693 imetatuliwa na kuhitimishwa kati ya migogoro 3,162 iliyopokelewa katika Mikoa 11 iliyofikiwa na Kampeni.
"Hizi takwimu wanaume ni wengi kuliko wanawake ni takwimu nzuri tu,unaona Mpango huu unamsaidia Mwananchi kuzalisha zaidi na programu hii ni mkombozi kwa wanyonge hasa wale ambao hawana uwezo wa kupata mawakili,"amesema Waziri Ndumbaro
Amesema Mpango huo unamsaidia mnyonge kupunguza malalamiko katika sekta ya sheria.
Aidha amesema Januari 24 mwaka huu watazindua kampeni hiyo kwa mikoa 6 Mkoani Kigoma.
Ameitaja mikoa mingine watakayofika ni,Kilimanjaro,Geita,Katavi,Tabora na Mtwara,
"Katika mikoa hiyo tutakuwa Januari tu na katika Kila Halmashauri wataenda Kata 10 katika Kila Kata watatumia siku 9 na huduma zitatolewa bure kwa wananchi,"amesema
Amesema wataanzia Januari 24 mkoani Kigoma kisha Katavi,Tabora na Mtwara ambapo Januari 25 watakuwa Geita na Januari 29 watamalizia Kilimanjaro.
Waziri Ndumbaro amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi ili waweze kupata msaada wa kisheria.
"Kampeni ya Msaada wa Kisheria ni mkombozi mkubwa kwa Wananchi Wanyonge na wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za Mawakili na mfumo mzima wa Sheria.Kupitia Kampeni hii Wanyonge wanasaidiwa kupunguza malalamiko katika sekta ya Sheria kwa kusimamia kikamilifu Sheria ya Utoaji Haki,"amesema.
Ameongeza kuwa kupitia kampeini hiyo wanatimiza Ilani ya CCM ambayo imefafanua kwa kina kila sekta jambo la kufanya na katika sekta yao ya utoaji haki imebainisha itakavyohakikisha wananchi wanapata haki kwa gharama nafuu na kwa wakati, wananpata elimu ya kisheria hivyo wao wanatekeleza ilani na kuwakumbusha kuwa Serikali imara haiishii kutekeleza hilo pekee. bali inaenda kulitengenezea nyaraka na muongozo wa kulitekeleza vyema.
DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDS
KAMATI ya Bunge ya miundombinu yaridhishwa na kasi ujenzi daraja la pangani
MIKOA 16 kunufaika na Nishati ya Jotoardhi
MASAA YA Upatikanaji wa Huduma ya Maji Yameongezeka Kutoka saa 16 hadi saa 22
MAMLAKA ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imefanikiwa kutoa mafunzo kwa wadau wa kemikali
Hatua Kali Za Kisheria Kuchukuliwa Kwa Watakaoghushi Cheti Cha Kuhitimu Mafunzo ya JKT.
Vituo 94 vimepewa mikopo na NHIF kwa ajili ya kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi.
RAIS SAMIA Aagiza Mamlaka Za Serikali za Mitaa Kujiepusha Kuwa Vyanzo vya Migogoro ya Ardhi Nchini.
NCAA IMEFANIKIWA Kudhibiti Ujangili wa Wanyamapori Ndani na Nje ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Mavunde Agawa Kompyuta na Printa kwa shule zote za Sekondari za Jiji la Dodoma.