

Serikali imeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ya viwanja vya ndege nchini ambapo Viwanja vya ndege vilivyokamilika ni,ujenzi na ukarabati wa kiwanja cha ndege cha Songwe, Mtwara, Songea, Iringa Awamu ya I na kiwanja cha ndege cha Geita.
Waziri wa Ujenzi Mhe.Abdallah Ulega ameyasema hayo Bungeni Jijini Dodoma tarehe 5 Mei 2025 wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara ya ujenzi kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
Aidha utekelezaji wa miradi mingine ya viwanja vya ndege ni Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato Package I (asilimia 87) na
Package II (asilimia 53.2); Kiwanja cha Ndege cha Kigoma (asilimia 20); Kiwanja cha Ndege cha Tabora (asilimia 93), Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga (asilimia 60), Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga (asilimia 80) na Kiwanja cha Ndege cha Musoma (asilimia 58).
Aidha katika mwaka wa fedha 2024/25, Wizara ya Ujenzi ilitengewa Shilingi 81,407,438,000.00 ikiwa ni Bajeti ya Matumizi ya
Kawaida,kati ya fedha hizo, Shilingi 76,588,233,000.00 ilikuwa ni Bajeti ya Mishahara na Shilingi 4,819,205,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo.
Hadi Aprili, 2025 jumla ya Shilingi 63,506,309,562.24 zilipokelewa,Kati ya fedha hizo, Shilingi 61,152,975,329.92 ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi wa Wizara na Taasisi na Shilingi 2,353,334,232.32 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo ya Wizara na Taasisi zake.
Bajeti kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo iliyotengwa kwa mwaka wa fedha 2024/25 kwa Wizara ya Ujenzi ni Shilingi 1,687,888,714,000.00. Kati ya fedha hizo, Shilingi 1,141,803,989,000.00 ni fedha za ndani na Shilingi 546,084,725,000.00 ni fedha za nje.
"Kati ya fedha za ndani, Shilingi 599,756,467,800.00 ni fedha zilizotengwa kwa ajili ya bajeti ya Mfuko wa Barabara na Shilingi
542,047,521,200.00 ni fedha kutoka katika Mfuko Mkuu wa Serikali"
"Hadi Aprili, 2025 fedha zilizopokelewa ni Shilingi 1,535,092,021,470.55. Kati ya fedha hizi, Shilingi 944,881,583,335.76 ni fedha za ndani na Shilingi 590,210,438,134.79 ni fedha za nje,kati ya fedha za ndani zilizopokelewa, Shilingi 482,085,328,011.98 ni kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali na Shilingi 462,796,255,323.78 ni za Mfuko wa Barabara"
Aidha Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS inasimamia mtandao wa barabara wenye urefu wa kilometa 37,435.04. Kati ya hizo kilometa
12,527.44 ni barabara kuu na kilometa 24,907.60 ni barabara za mikoa.
Katika mwaka wa fedha 2024/25, miradi ya barabara kuu iliyopangwa kutekelezwa ni ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara zenye urefu
wa kilometa 385, ukarabati wa kilometa 35 kwa kiwango cha lami, ujenzi wa madaraja 17, ukarabati wa daraja moja (1), maandalizi ya ujenzi wa madaraja tisa (9) na Upembuzi Yakinifu na Usanifu wa Kina wa madaraja mawili (2).
Hadi kufikia Aprili, 2025, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara zenye urefu wa kilometa 109.49 umekamilika na ujenzi wa kilometa
275.51 unaendelea.
Kwa upande wa madaraja, ujenzi wa madaraja matano (5) unaendelea na ujenzi wa madaraja matano (5) upo katika hatua za maandalizi,Vilevile, taratibu za ununuzi ya Makandarasi wa ujenzi wa madaraja matano (5)zinaendelea,Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa madaraja 11 na ukarabati wa daraja 1 katika mikoa mbalimbali nchini.
Sanjari na hayo hadi Aprili, 2025 jumla ya kilometa 98.13 za barabara za mikoa zilijengwa kwa kiwango cha lami na jumla ya kilometa 192.9 zilikarabatiwa kwa kiwango cha changarawe.
Aidha, ujenzi/ukarabati wa madaraja madogo 7 kwa kutumia fedha za Mfuko Mkuu wa Serikali na 9 kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara umekamilika na madaraja 91 yapo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
MKURUGENZI WA MASOKO TTB AELEZA FURSA INAYOWEZA KUPATA TANZANIA KUTOKA JAPAN KATIKA ELIMU YA UTALII NA UHIFADHI