MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya kusaidia watu wenye ulemavu ya mkoani Dodoma ya Foundation For Disabilities Hope (FDH), Maiko Salali amelipongeza Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira UNEP kwa jitiada zake za kupaisha agenda ya ulinzi wa mazingira kwa watu wenye Ulbino nchini.
Salali, amesema kupitia ushirikano wa shirika hilo la UNEP na FDH wameweza kusukuma Mpango kazi wa kitaifa wa haki na ustawi watu wenye ulbino ambapo serikali ilisikiliza na kufanyia kazi maombi hayo na hatimaye mpango huo umezinduliwa Desemba 03, 2024 katika siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu duniani.
“Kwa hapa Tanzania tuliazimisha katika ukumbi wa Dimond Jubilee Dar es salaam,ambapo FDH tunaishukuru sana UNEP kwa jitiada hizi ambazo zimewezesha watu wenye ulbino nchini kupata mpango, "
Na kuongeza kusema kuwa "Nimatumaini yetu kuwa tunaendelea kushirikiana ili kuendelea kuhakikisha agenda ya mazingira na ulinzi wa mazingira kwa watu wenye ulemavu unakuwa kipaumbele muhimu, " Amesema Salali
KOREA KASKAZINI YAWANASA ‘SNIPER’ UKRAINE, YADAI RUSSIA INAWAUA MAJERUHI
MAREKANI HALI TETE, MOTO WAUA 16 LOS ANGELES, UPEPO WATARAJIWA KUONGEZEKA
Ajali ya gari yajeruhi mamia ya watu Ufaransa
Maria Sarungi atekwa Kenya wasiojulikana watajwa
BENKI KUU YAWAGEUKIA WATENGENEZAJI, WAUZAJI ‘PUTTY’