

SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) limesema kuwa tukio lililotokea Novemba 3,2024 ambalo lilisababisha treni ya mchongoko (EMU) kusimama kwa takribani saa sita ni hujuma zilizohusisha kukatika ama kukatwa kwa nyaya (catenary) zinazochukua umeme kutoka njia ya umeme kupeleka kwenye treni.
Taarifa iliyotolewa leo Novemba 06,2024 na Mkuu wa Kitemgo cha Uhusiano TRC,Fredy Mwanjala imesema taarifa zilizosambaa kuwa treni hiyo ilizimika kutokana na changamoto za umeme si kweli kwakuwa hakuna treni ya mchongoko iliyopata hitilafu ya kiufundi.
“Tayari baadhi ya wahusika wamekamatwa na hatua stahiki dhidi yao zimeshaanza kuchukuliwa ikiwemo kufikishwa kwenye vyombo husika,tunawashukuru wenzetu wa TANESCO kwa ushirikiano mkubwa wanaoutoa,shirika linauhakikishia umma kuwa hakuna treni iliyopata hitilafu ya kiufundi,”amesema Mwanjala.
Amesema TRC imeutaka umma kupuuza taarifa potofu zinazosambazwa na watu mbalimbali na kwamba ukweli ni kuwa tangu kuanza kwa safari ya kwanza ya treni zinazotumia nishati ya umeme Juni 14, 2024 hakujawahi kuwa na changamoto ya umeme.
“Shirika linawakumbusha wananchi kuwa bado tuko kwenye kipindi cha mwaka mmoja cha matazamio, na kama changomoto zozote zinajitokeza, TRC itaujulisha umma kwa uwazi kama siku zote tunavyofanya, na taarifa rasm mtazipata kwenye vyanzo vyetu rasmi na si vinginevyo.,”amesema Mwanjala.
BODI YA MKONGE TANZANIA YATANGAZA FURSA KWA WATANZANIA.
SHERIA ZILIZOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI KUTOKA MWEZI AGOSTI.
DCEA:SERIKALI IMEPUNGUZA KASI YA WALAIBU WA DAWA ZA KULEVYA.
ULINZI NA USALAMA BAHARINI UMEIMARIKA;TASAC
VITONGOJI VYOTE 64,359 VITAKUWA NA UMEME IFIKAPO 2030
Maiko Salali achukua fomu ya ubunge Jimbo la Mpwapwa
SERIKALI IMEPUNGUZA TOZO KATIKA ZAO LA KAHAWA KUTOKA 17 HADI 5.
Mkoa wa Katavi umeendelea kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM)
UDOM KUJA NA TEKNOLOJIA MPYA YA KUUZA VIMIMINIKA.
AMANZI NA BABU TALE USO KWA USO JIMBONI