MRAJISI VYAMA VYA USHIRIKA AGUSWA NA HUDUMA YA MALIPO KWA MKUPUO YA TTCL. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Biashara

MRAJISI VYAMA VYA USHIRIKA AGUSWA NA HUDUMA YA MALIPO KWA MKUPUO YA TTCL.

MRAJISI wa vyama vya ushirika nchini Dkt Benson Ndiege ameipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa kuanzisha huduma ya malipo kwa mkupuo kwa vyama vya ushirika.

Sophia kingimali
By Sophia kingimali
08 Aug 2024
MRAJISI VYAMA VYA USHIRIKA AGUSWA NA HUDUMA YA MALIPO KWA MKUPUO YA TTCL.

Akizungumza mara baada ya kutembelea maonesho ya Wakulima Nanenane katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma amesema huduma hiyo imekuja wakati muafaka na itakuwa mkombozi kwa wakulima nchini.

"Kwenye vyama vya ushirika tuna vyama vya ushirika vya kilimo,kifedha madini vya mifugo na maeneo mengine yote kwa hiyo huduma hiyo itakuwa na tija kubwa",Amesema.

Amesema kwenye vyama vya ushirika kuna watu zaidi ya 500 ambao wanalima zao linalofanana hivyo wanapohitaji kulipana njia ya malipo ya mkupuo itawasaidia zaidi.

"Mfumo huu unaenda kuwasaidia vyama vyote vya ushirika kwani ni njia salama na ya kuaminika na itasaidia katika utendaji kazi",Amesema.

Aidha Dkt Ndiege ameongeza kuwa kutokana na umuhimu wa huduma hiyo wanapanga kukutana na uongozi wa TTCL na kuangalia jinsi huduma hiyo itakavyoenda kuwanufaisha vyama vya ushirika nchini.

WADAU WA UNUNUZI WAASWA KUZINGATIA MAADILI KAZINI

WADAU WA UNUNUZI WAASWA KUZINGATIA MAADILI KAZINI

TRA IMEWEZA Kushirikiana na Viongozi wa Vyama vya Wafanyabiashara Kujenga Mahusiano na Kutatua Changamoto.

TRA IMEWEZA Kushirikiana na Viongozi wa Vyama vya Wafanyabiashara Kujenga Mahusiano na Kutatua Changamoto.

Leseni 2,450 zatolewa na BoT kwa taasisi za mikopo daraja la pili

Leseni 2,450 zatolewa na BoT kwa taasisi za mikopo daraja la pili

WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU

WAZIRI MKUU WA UGANDA ASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA KUDUMU