

SERIKALI imesema itahakikisha inalinda miliki bunifu ili ziweze kusaidia kuondoa changamoto ndani ya jamii kwani maendeleo ya uchumi wa nchi yanategemea bunifu hizo.
SERIKALI imesema itahakikisha inalinda miliki bunifu ili ziweze kusaidia kuondoa changamoto ndani ya jamii kwani maendeleo ya uchumi wa nchi yanategemea bunifu hizo.
Akizungumza leo Mei 9,2024 Dar es Salaam katika maadhimisho ya siku ya miliki bunifu duniani,kwa niaba ya waziri wa Viwanda na biashara Dkt Ashatu Kijaja Naibu Waziri wa Utamaduni ,Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjumaa amesema serikali imeshaweka mazingira bora na wezeshi katika suala zima la biashara kwa kutumia miliki bunifu.
"Serikali inauhakika miliki bunifu itaondoa changamoto na kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja nchini hivyo ineweka mazingira wezeshi kwa kutumia bunifu katika biashara",Amesema.
Hata hivyo Naibu Waziri amewaelekeza BRELA kuhakikisha wamiliki Bunifu wanatambulika Kwa lengo la kuweza kukopeshwa na kunufaika katika kukuza biashara zao.
"Serikali inauwakika kuwa miliki bunifu zitaondoa chagamoto kwa jamii na zitaongeza ukuaji wa uchumi Kwa mtu mmoja mmoja,"alisema Naibu Waziri.
Mwinjuma amesema anatambua kazi nzuri inayofanya na BRELA katika kuwaimarisha wafanyabiashara na wenye makampuni kutekeleza shughuli zao za kimaendeleo.
"Tutahakikisha ifikapo mwaka 2030 kunakuwa na uwiano wa maendeleo duniani kwa kutumia miliki bunifu",amesema.
Amesema Serikali kwakushirikiana na Taasisi nyingine itawezesha ukamilikaji wa sera ya miliki bunifu ambayo italeta mwanga katika kusimamia mwongozo wa hati miliki Tanzania.
Aidha amesema Maadhimisho hayo yatumike kama fursa ya kujadili na kutoa maoni ambayo yatakayofanyiwa kazi.
Naye, Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA Godfrey Nyaisa amesema masuala ya ubunifu yatasaidia kusukuma ghurudumu la maendeleo mbele hivyo wana mpango wa kuanzisha programu ya miliki bunifu katika vyuo vyote nchini lengo ni kuendeleza ubunifu hizo na kuweza kutumika kwa maslahi ya nchi.
Aidha Nyaisa amesema nchi nyingi zinaendelea duniani kwa sababu ya kueneza miliki bunifu sehemu mbalimbali ndani ya nchi zao.
Nae Mwenyekiti wa bodi ya ushauri BRELA Profesa Neema Mboya amesema Maadhimisho hayo ni muhimu kuendelea kusheherekewa nchini kwani yanatoa fursa ya kukutanisha wadau mbalimbali na kuweza kujadiliana,kujifunza na kupata fursa ambazo zitasaidia kukuza bunifu za wabunifu nchini.
Amesema kufuatia maboresho yanayofanywa ndani ya BRELA yamepelekea kupokea wageni wengi kuja kujifunza wakiwemo Burundi pamoja na Sudani kusini.
RC MAKALLA AZINDUA MSIMU WA SHEREHE ZA MILA ZA KIMASAI
KAMATI YA ULINZI NA USALAMA TANGA YATOA ONYO KWA WATU WANAOPANGA KUVUNJA AMANI SIKU YA UCHAGUZI
JIJI LA DAR ES SALAAM NI SHWARI,JITOKEZENI KUPIGA KURA:RC CHALAMILA.
VIONGOZI WA DINI WAHIMIZA WATANZANIA KUPIGA KURA KWA AMANI.
BODABODA NA MACHINGA HATUTAKUWA CHANZO KUVUNJA AMANI YETU
PADRI NIKATA ALIJIPOTEZA KUTOKANA NA MSONGO WA MAWAZO NA KUACHWA NA MPENZI WAKE- POLISI
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
Vijana sasa kujifunza ufundi kwa urahisi kupitia programu ya VSOMO ya VETA
CHALAMILA: WATAKAOJIZIMA DATA OKTOBA 29, TUTAWAFANYA NETWORK ZISOME
RC MAKALLA AWAHAKIKISHIA USALAMA WAZEE WA MKOA WA ARUSHA SIKU YA UPIGAJI KURA OKTOBA 29.