

SERIKALI imesema itahakikisha inalinda miliki bunifu ili ziweze kusaidia kuondoa changamoto ndani ya jamii kwani maendeleo ya uchumi wa nchi yanategemea bunifu hizo.
SERIKALI imesema itahakikisha inalinda miliki bunifu ili ziweze kusaidia kuondoa changamoto ndani ya jamii kwani maendeleo ya uchumi wa nchi yanategemea bunifu hizo.
Akizungumza leo Mei 9,2024 Dar es Salaam katika maadhimisho ya siku ya miliki bunifu duniani,kwa niaba ya waziri wa Viwanda na biashara Dkt Ashatu Kijaja Naibu Waziri wa Utamaduni ,Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjumaa amesema serikali imeshaweka mazingira bora na wezeshi katika suala zima la biashara kwa kutumia miliki bunifu.
"Serikali inauhakika miliki bunifu itaondoa changamoto na kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja nchini hivyo ineweka mazingira wezeshi kwa kutumia bunifu katika biashara",Amesema.
Hata hivyo Naibu Waziri amewaelekeza BRELA kuhakikisha wamiliki Bunifu wanatambulika Kwa lengo la kuweza kukopeshwa na kunufaika katika kukuza biashara zao.
"Serikali inauwakika kuwa miliki bunifu zitaondoa chagamoto kwa jamii na zitaongeza ukuaji wa uchumi Kwa mtu mmoja mmoja,"alisema Naibu Waziri.
Mwinjuma amesema anatambua kazi nzuri inayofanya na BRELA katika kuwaimarisha wafanyabiashara na wenye makampuni kutekeleza shughuli zao za kimaendeleo.
"Tutahakikisha ifikapo mwaka 2030 kunakuwa na uwiano wa maendeleo duniani kwa kutumia miliki bunifu",amesema.
Amesema Serikali kwakushirikiana na Taasisi nyingine itawezesha ukamilikaji wa sera ya miliki bunifu ambayo italeta mwanga katika kusimamia mwongozo wa hati miliki Tanzania.
Aidha amesema Maadhimisho hayo yatumike kama fursa ya kujadili na kutoa maoni ambayo yatakayofanyiwa kazi.
Naye, Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA Godfrey Nyaisa amesema masuala ya ubunifu yatasaidia kusukuma ghurudumu la maendeleo mbele hivyo wana mpango wa kuanzisha programu ya miliki bunifu katika vyuo vyote nchini lengo ni kuendeleza ubunifu hizo na kuweza kutumika kwa maslahi ya nchi.
Aidha Nyaisa amesema nchi nyingi zinaendelea duniani kwa sababu ya kueneza miliki bunifu sehemu mbalimbali ndani ya nchi zao.
Nae Mwenyekiti wa bodi ya ushauri BRELA Profesa Neema Mboya amesema Maadhimisho hayo ni muhimu kuendelea kusheherekewa nchini kwani yanatoa fursa ya kukutanisha wadau mbalimbali na kuweza kujadiliana,kujifunza na kupata fursa ambazo zitasaidia kukuza bunifu za wabunifu nchini.
Amesema kufuatia maboresho yanayofanywa ndani ya BRELA yamepelekea kupokea wageni wengi kuja kujifunza wakiwemo Burundi pamoja na Sudani kusini.
EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA
SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3
SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA WALIMU 70,657 UTEKELEZAJI MITAALA ILIYOBORESHWA, YAANZA MAPITIO SHERIA YA ELIMU
DKT. DORIYE AVISHA VYEO VYA KIJESHI MAAFISA 145 NA ASKARI 476 WA NCAA NA KUSISITIZA UCHAPAKAZI, NIDHAMU, MAADILI NA UZALENDO KATIKA ULINZI WA RASILIMALI.
WAHUKUMIWA MIAKA 20 GEREZANI KWA KUHUJUMU MRADI WA ETDCO
Ibraah Afunguka: "Nilifukuzwa Konde Gang na Harmonize"
Watu Wenye Ulemavu Waomba Kuangaliwa kwa Jicho la Kipekee Katika Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.
Sekta ya Uvuvi imetoa ajira ya Moja Kwa Moja Kwa Wavuvi 201,661
BODI YA ITHIBATI YATAMBULISHWA RASMI BUNGENI
SERIKALI Imeendelea Kujenga na Kuboresha Miundombinu ya Viwanja vya Ndege