Ni Aibu Afrika Kulia Ukosefu wa Chakula-Rais Dkt. Samia | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kimataifa

Ni Aibu Afrika Kulia Ukosefu wa Chakula-Rais Dkt. Samia

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewakumbusha viongozi wa Afrika kuendelea kuwekeza katika Kilimo Biashara ili kulinusuru bara la Afrika kukumbwa na uhaba wa chakula kwani asilimia 65 ya ardhi Afrika inafaa kwa kilimo.

Gilbert Lordvick
By Gilbert Lordvick
07 Sep 2023
Ni Aibu Afrika Kulia Ukosefu wa Chakula-Rais Dkt. Samia

Kauli hiyo ameitoa Septemba 7, 2023 Jijini Dar es Salaam  wakati akihutubia Mkutano wa Jukwaa la Mifumo ya Chakula Afrika (AGRF 2023) mbele  ya marais kutoka nchi mbalimbali  kujadili  juu ya nini kifanyike kuboresha  mifumo  ya chakula Afrika.

Amesema Jukwaa hilo linatakiwa kuja na suluhu ya changamoto  ya chakula  na viongozi  wa Afrika wanatakiwa kuwa tayari kuhakikisha Afrika inajitosheleza kwa chakula.

"Asilimia 60 ni vijana ambao ni nguvu kazi, sisi viongozi  wa Afrika  tupo tayari  kuondoa aibu ya Afrika ya kuwa walalamikaji  tupo tayari kulisha Afrika na duniani  kwa ujumla," amesema Dkt. Samia.

Amesema licha ya rasilimali zilizopo, Afrika wamebaki kuwa walalamikaji baada  ya kutafuta suluhisho  kuelekea njia  ya mapinduzi ya uchumi wa kijani.

"Tupo na AGRF  washiriki wa maendeleo sekta binafsi wasomi na wataalamu kubadilishana uzoefu, namna  ya mnyororo wa thamani ya bidhaa za kilimo na kujadili  mipango  ya kuimarisha  usalama wa  Chakula Afrika," amesema.

Amesema, katika  kuelekea mageuzi wanayoyataka katika  sekta ya kilimo mataifa ya Afrika hayana budi kuweka mipango  na mikakati  kufikia Afrika wanayoitaka.

Aidha amesema  ili kufikia  malengo  viongozi wa Afrika  hawana budi kufanya tathmini  ya vipaumbele  vyao na kuvioanisha na mahitaji ya sasa katika muktadha wa dunia.

Amesema  zaidi  ya watu milioni  283 wanalala njaa Barani Afrika hivyo wanatakiwa kutathmini mambo ya muhimu ili kuboresha kilimo kulikomboa bara la Afrika dhidi ya baa la njaa. 
 
Naye Rais  wa Jamhuri ya  Kenya, William Ruto amesema  ardhi  ya kilimo  ipo  Afrika hivyo mkutano  huo wa AGRF  ni somo  kubwa, Teknolojia na muda vinahitajika ili kuweza kupata chakula cha kutosha kwenye bara la Afrika hata kupeleka Duniani.

"Tunaweza kuchochea  biashara  ya kilimo kuacha kuwa watu wa  kulalamika wakati ardhi  tunayo  ni suala  la kuongeza  uzalishaji na kufikiria  tunafanyeje wakulima wazalishe zaidi," amesema Rais Ruto.

Amesema  katika  somo la mkutano  huo wa AGRF  ni jinsi gani  watafanya mabadiliko ili kubadilisha    wakulima waweze kuzalisha kwa wingi ili gharama za chakula zipungue barani Afrika.

Profesa Malebo:Tanzania  inatoa uhuru wa kujieleza na hakuna vitisho wala unyanyasaji wa wananchi

Profesa Malebo:Tanzania inatoa uhuru wa kujieleza na hakuna vitisho wala unyanyasaji wa wananchi

MPANGO afungua mkutano wa kumi wa wakaguzi wa ndani Afrika

MPANGO afungua mkutano wa kumi wa wakaguzi wa ndani Afrika

RAIS DKT.SAMIA AANDALIWA DHIFA YA KITAIFA NORWAY

RAIS DKT.SAMIA AANDALIWA DHIFA YA KITAIFA NORWAY

Mwaimu Akutana na Kuzungumza na Ujumbe wa Balozi wa USA Nchini

Mwaimu Akutana na Kuzungumza na Ujumbe wa Balozi wa USA Nchini

DKT Mpango Atoa Wito kwa Serikali za Afrika Kusaidia Wakulima Kuongeza Uzalishaji Chakula

DKT Mpango Atoa Wito kwa Serikali za Afrika Kusaidia Wakulima Kuongeza Uzalishaji Chakula