TUME YA UCHAGUZI YAONYA WANAOSHAWISHI KUTOPIGA KURA “NI KOSA KISHERIA’ | The Dodoma Post
The Dodoma Post Tanzania

TUME YA UCHAGUZI YAONYA WANAOSHAWISHI KUTOPIGA KURA “NI KOSA KISHERIA’

Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhan Kailima, amewatahadharisha wananchi na wadau wa siasa nchini kuwa kuhamasisha watu kutoshiriki kupiga kura ni kosa la kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
16 Oct 2025
TUME YA UCHAGUZI YAONYA WANAOSHAWISHI KUTOPIGA KURA “NI KOSA KISHERIA’

Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhan Kailima, amewatahadharisha wananchi na wadau wa siasa nchini kuwa kuhamasisha watu kutoshiriki kupiga kura ni kosa la kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024.

Akizungumza katika mahojiano maalum na kituo cha televisheni cha UTV, Kailima amesema kifungu cha 129 cha sheria hiyo kinaeleza wazi kuwa mtu yeyote anayetumia nguvu, vitisho, au udanganyifu kumshawishi mpiga kura kuacha kupiga kura anatenda kosa la ushawishi mbaya, na anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria.

Amefafanua kuwa kifungu hicho kinakataza mtu yeyote kutumia au kutishia kutumia nguvu, vurugu, au hila ya aina yoyote kwa lengo la kumshawishi mpiga kura kupiga au kuacha kupiga kura, akisisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa kwa watakaobainika kuvunja masharti hayo.

MRADI WA HEET WAFUNGUA UKURASA MPYA WA MAGEUZI KATIKA ELIMU NCHINI.

MRADI WA HEET WAFUNGUA UKURASA MPYA WA MAGEUZI KATIKA ELIMU NCHINI.

WANNE JELA MIAKA SABA KWA JARIBIO LA KUMTEKA MFANYABIASHARA

WANNE JELA MIAKA SABA KWA JARIBIO LA KUMTEKA MFANYABIASHARA

TUNALAANI WOTE WANAOHAMASISHA MAANDAMANO- MALAIGWANAN K'NJARO

TUNALAANI WOTE WANAOHAMASISHA MAANDAMANO- MALAIGWANAN K'NJARO

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA TANGA YATOA ONYO KWA WATU WANAOPANGA KUVUNJA AMANI SIKU YA UCHAGUZI

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA TANGA YATOA ONYO KWA WATU WANAOPANGA KUVUNJA AMANI SIKU YA UCHAGUZI

JWTZ NA POLISI MOROGORO WAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUJIIMARISHA KATIKA ULINZI NA USALAMA

JWTZ NA POLISI MOROGORO WAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUJIIMARISHA KATIKA ULINZI NA USALAMA