MWENYEKITI WA BODI YA T-PESA AWATAKA WANANCHI KUWA WAZALENDO. | The Dodoma Post
The Dodoma Post Biashara

MWENYEKITI WA BODI YA T-PESA AWATAKA WANANCHI KUWA WAZALENDO.

Mwenyekiti wa bodi ya T Pesa kutoka Shirika mawasiliano Tanzania TTCL Richard Mayongela ametoa rai kwa wananchi kutumia huduma zinazozalishwa nchini ili kuchochea maendeleo lakini kukuza uchumi wa Taifa.

Sophia Kingimali.
By Sophia Kingimali.
07 Aug 2024
MWENYEKITI WA BODI YA T-PESA AWATAKA WANANCHI KUWA WAZALENDO.

Wito huo ameutoa leo jijijni Dodoma kwenye maonesho ya Nanenane Nzuguni wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea banda la Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL lililopo kwenye maoneshe hayo.

Amesema kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali katika shirika hilo umepelekea kuwepo na huduma bora zinazotolewa na shirika kwa umma.

"Wito wangu kwa watanzania na wadau tutumie vilivyo vyetu nyumbani kumenoga TTCL ni shirika la umma kwa hiyo wanapolitumia tunarejesha faida  kwa wananchi wenyewe",Amesema.

Amesema kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika sasa hivi wamepeleka huduma ya internet kwenye majengo ya serikali lakini pia huduma ya fiber Mlangoni sasa inapatikana ambapo mteja anapelekewa huduma hiyo mpaka kwenye makazi yake.

Aidha ameongeza kuwa TTCL imeendelea kusambaza huduma za mawasiliano katika vyuo na taasisi mbalimbali za umma.

"Tunashukuru serikali kwa uwekezaji mkubwa ambao umeufanya kwa miaka ya hivi karibuni sasa shirika linaweza kuwafikia wateja kwenye nyanja mbalimbali ambapo sasa hivi tumeanza kwenye kilimo na biashara",amesema.

Akizungumzia huduma ya lipa kwa mkupuo amesema shirika limekuja na huduma hiyo kwa madhumuni ya kurahisisha malipo kwa wakulima,wafanyabiashara na wadau mbalimbali ambao wanahitaji kuwalipa watu wengi.

"Shirika limekuja na huduma hii kwa madhumuni ya kurahisisha malipo badala ya mtu kubeba pesa na kumlipa mtu mmoja mmoja sasa unaweza kulipa wote kwa mkupuo",Amesema.

VIONGOZI SOKO LA MACHINGA DODOMA WASIMAMISHWA KUPISHA UCHUNGUZI

VIONGOZI SOKO LA MACHINGA DODOMA WASIMAMISHWA KUPISHA UCHUNGUZI

BRELA YAWATAKA WASANIFU MAJENGO NA WAJASIRIAMALI KUTUMIA VIZURI BUNIFU ZAO.

BRELA YAWATAKA WASANIFU MAJENGO NA WAJASIRIAMALI KUTUMIA VIZURI BUNIFU ZAO.

MCHENGERWA AZINDUA MFUMO WA KADI JANJA ZA MWENDOKASI AWATAKA DART NA UDART KUTATUA CHANGAMOTO YA UHABA WA MAGARI.

MCHENGERWA AZINDUA MFUMO WA KADI JANJA ZA MWENDOKASI AWATAKA DART NA UDART KUTATUA CHANGAMOTO YA UHABA WA MAGARI.

MRAJISI VYAMA VYA USHIRIKA AGUSWA NA HUDUMA YA MALIPO KWA MKUPUO YA TTCL.

MRAJISI VYAMA VYA USHIRIKA AGUSWA NA HUDUMA YA MALIPO KWA MKUPUO YA TTCL.

PPAA YAOKOA BILIONI 567.6 KATIKA MICHAKATO YA ZABUNI ZA UMMA

PPAA YAOKOA BILIONI 567.6 KATIKA MICHAKATO YA ZABUNI ZA UMMA