Msaada wa kisheria Kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

Msaada wa kisheria Kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla amesema kampeni ya huduma ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia inalenga kulinda na kukuza upatikanaji wa haki kupitia huduma za msaada wa kisheria Nchini.

Mwandishi Wetu
By Mwandishi Wetu
06 Jun 2023
Msaada wa kisheria Kwa Haki, Usawa, Amani na Maendeleo

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla amesema kampeni ya huduma ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia inalenga kulinda na kukuza upatikanaji wa haki kupitia huduma za msaada wa kisheria Nchini.

Ameyasema hayo wakati akizindua kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Mkoa wa Mjini Magharibi katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar. 

Ameeleza kuwa kampeni hiyo itaimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi wasiojiweza, wanawake, watoto pamoja na makundi mengine yanayoishi katika mazingira magumu, kuimarisha amani na utulivu na kuleta utengamano wa Kitaifa.

Sambamba na hayo Hemed amewaagiza wanaohusika na utekelezaji wa Kampeni hiyo kutekeleza majukumu yao ipasavyo ili kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi za kupiga vita na kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia, udhalilishaji na migogoro ya ardhi vitendo ambavyo vimekua vikijitokeza katika jamii.

Aidha amewapongeza wadau mbali mbali wakiwemo Wasaidizi wa Sheria, Jeshi la Polisi, Mahkama, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka kwa kuhakikisha kila mwananchi anapata haki yake kwa mujibu wa Sheria juhudi ambazo zinaleta taswira njema kwa Wananchi kuwa na imani na wadau hao.

Naye waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Harun Ali Suleiman amesema Kampeni hiyo itasaidia kupunguza dhulma, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia katika jamii.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Idriss Kitwana Mustafa amesema Serikali ya Mkoa itakuwa karibu na wananchi katika kuhakikisha kampeni hiyo inafanikiwa ipasavyo kwa lengo la kumuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Samia na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Mwinyi.

Kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia imezinduliwa June 6, 2023 kwa lengo la kuwafikia wananchi hasa wasio na uwezo ikiwa na kauli mbiu isemeyo “Msaada wa kisheria kwa haki, usawa, amani na maendeleo”

MWENYEKITI CHADEMA WILAYA YA MWANGA AMTAKA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUTENGUA MAAMUZI YA BARAZA KUU LA CHAMA HICHO.

MWENYEKITI CHADEMA WILAYA YA MWANGA AMTAKA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA KUTENGUA MAAMUZI YA BARAZA KUU LA CHAMA HICHO.

WMA IMEJENGA MAJENGO MAPYA YA OFISI MKOA WA MARA NA SIMIYU

WMA IMEJENGA MAJENGO MAPYA YA OFISI MKOA WA MARA NA SIMIYU

COSOTA IMETOA JUMLA YA VYETI  7,679 VYA UDHIBITISHO WA UMILIKI WA HAKIMILIKI KWA WABUNIFU

COSOTA IMETOA JUMLA YA VYETI 7,679 VYA UDHIBITISHO WA UMILIKI WA HAKIMILIKI KWA WABUNIFU

Serikali Imeiwezesha NIT Kukamilisha Maandalizi ya Utoaji wa Mafunzo ya Urubani Kwa Gharama za Shilingi Bilioni 6.

Serikali Imeiwezesha NIT Kukamilisha Maandalizi ya Utoaji wa Mafunzo ya Urubani Kwa Gharama za Shilingi Bilioni 6.

HAKUNA SHERIA INAYOMKATAZA MWANAMKE KUMILIKI ARDHI:RAIS SAMIA

HAKUNA SHERIA INAYOMKATAZA MWANAMKE KUMILIKI ARDHI:RAIS SAMIA