

Jeshi la Polisi nchini limesema litaendelea kufuatilia kwa kina, kuzuia, kubaini na kutanzua matishio yoyote ya usalama kuelekea siku ya upigaji kura ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.
Jeshi la Polisi nchini limesema litaendelea kufuatilia kwa kina, kuzuia, kubaini na kutanzua matishio yoyote ya usalama kuelekea siku ya upigaji kura ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.
Akizungumza leo Oktoba 15, 2025 jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Jumanne Muliro, alisema jeshi hilo limejipanga ipasavyo kuhakikisha amani, utulivu na usalama vinatawala kabla, wakati na baada ya uchaguzi
“Tunataka wananchi wajitokeze kwa wingi kushiriki uchaguzi bila hofu yoyote. Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kulinda usalama wa watu na mali zao, hivyo hakuna sababu ya mtu kuogopa,” alisema Kamanda Muliro.
Amesema vikosi vyote vya ulinzi na usalama viko katika tahadhari ya hali ya juu, huku jeshi likiendelea kufuatilia mitandao ya kijamii na maeneo mbalimbali ili kubaini dalili zozote za uchochezi au mipango ya uvunjifu wa amani.
Aidha, amewataka wananchi kuepuka kusambaza taarifa za uzushi mitandaoni na badala yake watoe ushirikiano kwa vyombo vya dola kwa kutoa taarifa sahihi pale wanapobaini vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa taifa.
Muliro ameongeza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea kushirikiana na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na wadau wengine kuhakikisha mazingira yote yanabaki salama hadi kukamilika kwa zoezi la uchaguzi.
TUNAAMINI UCHAGUZI UTAKUWA WA AMANI NA USALAMA UTAKUWEPO- WANANCHI WA KIBAHA
RC MAKALLA AWAHAKIKISHIA USALAMA WAZEE WA MKOA WA ARUSHA SIKU YA UPIGAJI KURA OKTOBA 29.
Mfalme wa Mashairi Awasha Moto wa Uzalendo: “Kura Yako Ni Silaha”
MUFTI ATAKA WAISLAMU KUZINGATIA MAFUNDISHO YA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29.
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
BRIGEDIA JENERALI NDAGALA AFUNGUA KONGAMANO LA WADAU WA USIMAMIZI WA MAAFA JIJINI MBEYA
Mkomi Awasisitiza Wakuu wa Taasisi Kusimamia Mifumo ya Kielektroniki Serikalini.
WAZEE WAASWA KUHAMASISHA JAMII KUJITOKEZA KUPIGA KURA.
DOWOSA Yawaokoa Wanawake Dodoma Kutoka Mikononi mwa “Kausha Damu”
TUMEJIANDAA VYEMA KUDHIBITI UHALIFU NA WAHALIFU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU- POLISI