

Ujenzi wa nyumba mbili za kisasa kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum (wasiojiweza) katika kata za Kitobo na Minziro, wilayani Missenyi, Mkoani Kagera, umeingia hatua za mwisho.
Nyumba hizo zilizojengwa na Evance Kamenge ambaye ni mchumi na mkulima ni mfano wa kipekee wa msaada wa kijamii unaotolewa kwa moyo wa dhati.
Kamenge, akielezea nia yake ya kujenga nyumba hizi, amesema aliguswa na maisha magumu wanayoishi wakazi wa maeneo hayo ndipo aliamua kuchukua hatua.
Kwa mujibu wa Kamenge nyumba hizo zitakamilika mwishoni mwa mwezi Juni 2025, ambapo zitakabidhiwa kwa walengwa.
Katika juhudi zake za kusaidia jamii, Kamenge amejenga nyumba hizo kutokana na vyanzo vyake vya mapato na kwa ushirikiano na marafiki zake wa karibu ambao ni wadau wa maendeleo.
Aidha amewaomba wananchi wengine kuchukua hatua kama hiyo huku akisisitiza kuwa kusaidia jamii hakuhitaji mtu kuwa kiongozi, bali inahitaji mapenzi ya dhati ya kusaidia wale walio katika mahitaji.
Moja ya wanufaika, kutoka eneo la Minziro akiwemo Biteganya Mbili amemshukuru Kamenge kwa nyumba hiyo ya kisasa yenye vyumba vitatu na kuahidi kuwa ataendelea kumuombea Kamenge kwa mwenyezi Mungu ili amuongezee neema na baraka,
Mdau huyo amewashukuru wadau wengine walioshirikiana katika msaada huo.
Evance Kamenge ni mzaliwa wa kata ya Kanyigo wilayani Missenyi Mkoani Kagera ameonyesha mfano wa kujitolea katika shughuli za maendeleo bila kujali eneo husika.
Hata hivyo Ujenzi wa nyumba hizo unaleta matumaini ya maisha bora kwa walengwa.
Rais Samia Asisitiza Mchujo wa Wagombea Kufanyika Kwa Haki.
Ilani Ya CCM Imeandaliwa Kwa Weledi Mkubwa Kwa Kushirikiana Na Wananchi;RAIS Dkt.Samia
WIZARA YA ARDHI YAJA NA VIPAUMBELE SABA
SERIKALI NA WADAU WAENDELEZA MAPAMBANO YA KIJINSIA
KAPINGA ATAJA VIGEZO VYA ZIADA UPELEKAJI UMEME VITONGOJINI.