EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA | The Dodoma Post
The Dodoma Post Kijamii

EVANCE KAMENGE AJITOLEA KUSAIDIA JAMII KAGERA

Ujenzi wa nyumba mbili za kisasa kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum (wasiojiweza) katika kata za Kitobo na Minziro, wilayani Missenyi, Mkoani Kagera, umeingia hatua za mwisho.

Lydia Lugakila
By Lydia Lugakila
13 May 2025
EVANCE KAMENGE AJITOLEA  KUSAIDIA JAMII KAGERA

Nyumba hizo zilizojengwa na Evance Kamenge ambaye ni mchumi na mkulima ni mfano wa kipekee wa msaada wa kijamii unaotolewa kwa moyo wa dhati.

Kamenge, akielezea nia yake ya kujenga nyumba hizi, amesema aliguswa na maisha magumu wanayoishi wakazi wa maeneo hayo ndipo aliamua kuchukua hatua.

Kwa mujibu wa Kamenge  nyumba hizo zitakamilika mwishoni mwa mwezi Juni 2025, ambapo zitakabidhiwa kwa walengwa.

Katika juhudi zake za kusaidia jamii, Kamenge amejenga nyumba hizo kutokana na vyanzo vyake vya mapato na kwa ushirikiano na marafiki zake wa karibu ambao ni wadau wa maendeleo.

Aidha amewaomba wananchi wengine kuchukua hatua kama hiyo huku akisisitiza kuwa kusaidia jamii hakuhitaji mtu kuwa kiongozi, bali inahitaji mapenzi ya dhati ya kusaidia wale walio katika mahitaji.

Moja ya wanufaika, kutoka eneo la Minziro akiwemo Biteganya Mbili amemshukuru Kamenge kwa nyumba hiyo ya kisasa yenye vyumba vitatu na kuahidi kuwa ataendelea kumuombea Kamenge kwa mwenyezi  Mungu ili amuongezee neema na baraka,

Mdau huyo amewashukuru wadau wengine walioshirikiana katika msaada huo.

Evance Kamenge ni mzaliwa wa kata ya Kanyigo wilayani Missenyi Mkoani Kagera ameonyesha mfano wa kujitolea katika shughuli za maendeleo bila kujali eneo husika.

Hata hivyo Ujenzi wa nyumba hizo unaleta matumaini ya maisha bora kwa walengwa.

SERIKALI NA WADAU WAENDELEZA MAPAMBANO YA KIJINSIA

SERIKALI NA WADAU WAENDELEZA MAPAMBANO YA KIJINSIA

Siku Ya Utumishi wa Umma, Watumishi Kufanya Maonesho ya Kutambua Mchango na Umuhimu wao Kwenye Jamii.

Siku Ya Utumishi wa Umma, Watumishi Kufanya Maonesho ya Kutambua Mchango na Umuhimu wao Kwenye Jamii.

Vijana Kutoka Kenya Waonywa Vikali Kuacha Kumkejeli Rais Samia Katika Mitandao ya Kijamii

Vijana Kutoka Kenya Waonywa Vikali Kuacha Kumkejeli Rais Samia Katika Mitandao ya Kijamii

Wizara Imetekeleza Mradi wa Uboreshaji wa Usalama wa Milki za Ardhi(LTIP)

Wizara Imetekeleza Mradi wa Uboreshaji wa Usalama wa Milki za Ardhi(LTIP)